Mimi sio mjinga, nimeamua kuzungumza-mwanamke aliyelaghaiwa kimapenzi kwa miaka tisa

Amber Sandhu na Manish Pandey

BBC Asian Network News

th

Chanzo cha picha, NETFLIX

Maelezo ya picha, Kirat Assi alilaghaiwa kimapenzi kwa karibu miaka tisa

Yote ilianza na ombi la urafiki.

Kirat Assi alifikiri amepata 'dhahabu' wakati Bobby, daktari mtanashati wa magonjwa ya moyo, alipowasiliana naye mwaka wa 2009.

Hakuwa mgeni kabisa. Wawili hao wote walitoka jamii ya Sikh ya London magharibi na walikuwa na marafiki sawa.

Kwa hivyo, Kirat alikubali, na mazungumzo yake ya mtandaoni yalikua mazungumzo ya kina kabla ya kugeuka na kuwa hadithi ya mapenzi.

Wawili hao waliingiana zaidi katika maisha ya kila mmoja wao lakini hawakuwahi kukutana, hata baada ya miaka mingi ya mawasiliano.

Bobby alitoa visingizio vya ajabu zaidi. Alikuwa na kiharusi. Alikuwa amepigwa risasi. Alikuwa ameingia kwenye mpango ulinzi wa mashahidi.

Hadithi ndefu, ingawa, ziliungwa mkono na mtu wa karibu wa Bobby - au hivyo ndivyo Kirat alivyofikiria.

Kwa kweli, alikuwa mwathirika wa mpango kabambe sana na wa kutisha wa kulaghaiwa kimapenzi katika mtandao au Catfishing kwa Kiingereza .

Baada ya miaka tisa, visingizio vilipopungua, hatimaye Kirat alikutana uso kwa uso na Bobby.

Lakini hakumtambua mtu aliyekuwa mbele yake.

Mtu ambaye alikuwa akimtumia ujumbe alikuwa binamu yake wa kike, Simran, ambaye ndiye alikuwa mhusika wa kila kitu nyuma ya pazia.

Akikumbuka sasa, Kirat anajiuliza: "Niliwezaje kuwa mjinga sana");