Mfahamu mkimbizi wa Afghanistan anayeongoza jeshi la Ukraine
Jalal Noory alikuwa mtoto mdogo alipotoroka vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Afghanistan kufuatia uvamizi wa Kisovieti katika nchi yake, Afghanistan mwaka 1979.
Aliishia Ukraine na ikawa nyumba yake ya pili ambako alijijengea 'maisha ya mafanikio'.
Miaka 24 baadaye aliamka akishuhudia uvamizi wa Warusi nchini Ukraine na alikuwa na chaguo mbili tu: 'kutetea au kufa.'