Hizi ni dhana 7 za unyonyeshaji unazopaswa kuzijua

Chanzo cha picha, Getty Images
Umoja wa Mataifa, ikiwa ni sehemu ya kampeni yake ya kila mwaka ya kuongeza viwango vya unyonyeshaji, unatoa wito wa kuungwa mkono zaidi kwa wanawake kunyonyesha mahali pa kazi. Ikilinganishwa na watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama pekee, watoto ambao hawajanyonyeshwa maziwa ya mama wana uwezekano wa kufa mara 14 kabla ya kutimiza mwaka mmoja, shirika hilo linasema.
Umoja wa Mataifa unatoa wito kwa akina mama kupewa likizo ya uzazi yenye malipo, mapumziko kwa ajili ya kunyonyesha, na chumba maalumu mahali pa kazi ambapo wanaweza kunyonyesha.
Kuna simulizi na dhana nyingi kuhusu unyonyeshaji bado zipo katika jamii, ambayo inaweza kuwapa majaribu wanawake kutonyonyesha. Tuliuliza wataalam wawili kufafanua baadhi ya dhana hizi.
Cathriona Waite ni Profesa wa Kliniki Pharmacology na Afya Ulimwenguni katika Chuo Kikuu cha Liverpool na Mtafiti Wenzake katika Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya cha Mackayre, Kampala, Uganda. Alastaira Sutcliffe ni Profesa wa Madaktari Mkuu wa Watoto katika Chuo Kikuu cha London London.
Walitufafanulia dhana saba zinazoonekana ni za kawaida katika jamii.
1. Maumivu ya kunyonyesha
Prof. Waite: Hili ni gumu kidogo kujibu kwa sababu ni kawaida kuhisi usumbufu mwanzoni, na ni kawaida chuchu kuuma mwanzoni kabla ya kuzoea [kunyonyesha]. Hata hivyo, kunyonyesha si lazima iendane na maumivu au kusababisha maumivu makali. [Ukihisi hivyo] ina maana kwamba chuchu zimeambukizwa au mtoto hajanyonya ipasavyo.
Ni kawaida kuhisi usumbufu [wakati wa kunyonyesha], na kunyonyesha kunahitaji kuzoea, haswa kwa akina mama wanaonyonyesha. Lakini ikiwa husababisha maumivu, unapaswa kumjulisha daktari wako, muuguzi au afisa wa afya wa familia kuhusu hilo.

Chanzo cha picha, Getty Images
2. Ikiwa unyonyeshaji haujaanza mara moja, huenda isiwezekane kunyonyesha baadaye
Profesa Sutcliffe: Kitu chochote kinachohimiza akina mama kunyonyesha ni kizuri kwa afya ya binadamu katika viwango vingi.
Lakini kuna faida nyingi za kuanza kumnyonyesha mtoto mara tu baada ya kujifungu.
Faida dhahiri zaidi ni lishe. Kupitia hiyo, mchakato wa uterasi pia huanza. Hii husaidia kuzuia au kupunguza kasi ya damu ya mfuko wa uzazi baada ya kujifungua. Pia, katika siku chache za kwanza baada ya kujifungua, mwili wa binadamu hzalisha kitu kinachoitwa 'colostrum', ambayo ina protini nyingi na za kipekee. Ni lishe muhimu sana katika siku za mwanzoni mwa kunyonyesha.

Chanzo cha picha, Getty Images
3. Huwezi kutumia dawa yoyote wakati wa kunyonyesha
SahProfesa Waite: Hili ni swali la kwanza ambalo mama anauliza popote ulimwenguni. 'Je, kuna dawa salama kwa mtoto wangu'? Kwa kweli, dawa nyingi hutolewa kwa watoto wachanga katika viwango vya chini sana. Ikiwa daktari anasema unahitaji kunywa dawa, waulize swali lako. Lakini dawa hiyo labda ni salama kutumia. Mama mwenye afya ndiye kile ambacho mtoto anahitaji zaidi. Dawa za kawaida za maambukizo, uchovu na maumivu ya jumla mara nyingi ni salama. Dawa unazohitaji kuwa makini nazo, kwa kawaida ni dawa za kukohoa, baridi na pua - zinaweza kupunguza mtiririko wa maziwa. Pia, daima kuwa makini na dawa za mitishamba, kwa sababu hatujui ni nini kimo ndani yake.

Chanzo cha picha, Getty Images
4. Kabla ya kunyonyesha, kula chakula chenye viungo kidogo ama kisicho na viungo kabisa
Prof. Waite: Hakuna vyakula ambavyo havifai kuliwa wakati wa kunyonyesha. lakini, utengenezwaji wa maziwa ya mama huathiriwa na lishe yako. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kuchunguza kwa mfano - niliona hili kutoka kwa mmoja wa watoto wangu - ikiwa nitawahi kunywa kinywaji cha machungwa kama juisi ya machungwa, [baada ya kunywa maziwa ya mama] mtoto wangu angepatwa na kitu fulani. Wakati mwingine ni lazima kiwe na madhara au kibaya kiafya, jambo ambalo unapaswa kuepuka.

Chanzo cha picha, Getty Images
5. Ikiwa unataka kunyonyesha, hupaswi kumchanganyia mtoto maziwa mengine
Profesa Waite: Hakuna ukweli kamili kwenye hili. Hata hivyo, upatikanaji wa maziwa ya mama kwa kiasi kikubwa yanategemea yanavyozalishwa na mahitaji. Mwili wa mwanamke umeundwa kwa njia ya ajabu ili kutoa maziwa ya kutosha kwa mtoto wake. Wakati mtoto ananyonya kwenye chuchu, homoni huchochewa na kiasi kinachofaa cha maziwa hutolewa. Kwa hiyo, iwe unanyonyesha mtoto mdogo, mtoto mkubwa au mapacha, mwili wako utazalisha maziwa ya kutosha.
Ukianza kulisha maziwa ya mtoto wako, mzunguko huu wa mahitaji ya usambazaji unatatizwa. Kisha mwili wako haupati ishara za kutosha kwamba mtoto anahitaji maziwa zaidi. Ukianza kumpa maziwa mengine mtoto wako (formula) kwa sababu maziwa yako ni kidogo, inaweza kukupa nafuu ya muda mfupi, lakini matatizo yako yanaweza kuanza kuwa mabaya zaidi.
Lakini kwa upande mwingine, ukiwa na usiku mbaya pengine unaumwa, au umechoka sana, kwa sababu mtoto anakunywa maziwa mengine, haimaanishi hutaweza kunyonyesha tena. Kwa hivyo, inaweza isiwe jambo linalosisitizwa, lakini inaweza kuwa sio faida

Chanzo cha picha, Getty Images
6. Epuka kunyonyesha ikiwa unaumwa
Profesa Sutcliffe: Hapana, ni uongo. Wakati pekee ambao mwanamke anapaswa kuepuka kunyonyesha ni ikiwa ana VVU au homa ya ini. Virusi vinaweza kuambukizwa kupitia maziwa ya mama. Tumepitia hali hii ya kusikitisha huko nyuma.
Katika hali nyingi, ni salama kuendelea kunyonyesha hata kama mama ni mgonjwa, kwa sababu kingamwili zinazozalishwa na mwili wa mama hulinda mtoto wake mchanga. Ni nadra sana kwamba ugonjwa wa mtoto hupitishwa kutoka kwa mama kupitia maziwa ya mama.

Chanzo cha picha, Getty Images
7. Ikiwa unanyonyesha mtoto kwa zaidi ya mwaka mmoja, inakuwa vigumu kwa mtoto kunyonya
Profesa Waite: Mapendekezo ya Shirika la Afya Ulimwenguni ni kwamba unapaswa kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa miezi sita. Hata baada ya hapo, hata kama njia nyingine za lishe (chakula) zitaanzishwa, shirika hilo linapendekeza kwamba uendelee kumnyonyesha mtoto kwa muda unaohitaji. Hakuna wakati unaopendekezwa kwako kuacha kufanya hivyo.
Katika baadhi ya nchi zenye kipato cha juu kama vile Uingereza, watoto wengi wameachishwa kunyonya kabisa kati ya umri wa mwaka mmoja na miwili. Wakati huo huo, katika nchi zenye kipato cha chini kama Uganda, watoto wananyonyeshwa hadi wanafikisha umri wa miaka miwili au mitatu. Tatizo la kimataifa hapa ni kwamba kulingana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani, akina mama katika nchi nyingi hawapewi likizo ya uzazi kwa muda wa kutosha kuweza kunyonyesha mtoto.