Waridi wa BBC: 'Mambo ni mawili, umrushe mtoto mtoni au niwauwe nyote wawili'

.
  • Author, Na Asha Juma
  • Nafasi, BBC Swahili Nairobi

Kila anapokumbuka usiku ule wa kutisha, Marion Watswenje anajihisi kama mtu aliyefufuka kutoka kaburini. Alishtuliwa kutoka usingizini na maneno ambayo yangeweza kuwa ya utani, lakini hayakuwa hivyo.

"Aliniamsha usiku wa manane akaniambia, unaona ule mto unaoitwa Riverside, siku moja nitaamka na wewe hapa nikakutumbukize humo ndani."

Siku iliyofuata, saa sita za usiku, aliamshwa tena. Mara hii si kwa maneno ya kutisha tu, bali kwa kitendo kilichomuweka ukingoni mwa maisha na mauti.

"Nikambeba mtoto mgongoni. Akaniambia tunaenda hospitali. Tulipofika kwenye mto, alinigeukia na kusema, hapa ndipo maisha yenu yanaishia. Mambo ni miwili, umrushe mtoto mtoni au niwaue nyote wawili."

Kauli hii ya mume wake aliyosheheni maneno mazito ilibadili kabisa mtazamo wake wa maisha hadi leo.

Katika simulizi hii, Marion Watswenje anasimulia jinsi ndoa yake ilivyogeuka kuwa jinamizi na namna kifo kilivyomkabili usoni.

Tahadhari: Baadhi ya simulizi inaweza kukuumiza moyo

Karibu.

Ruka YouTube ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje Mitandao ya kijamii inaweza beba matangazo

Mwisho wa YouTube ujumbe

Safari ya maisha yake ni hadithi ya simanzi

Marion, alimpoteza mama yake mzazi mnamo mwaka 1997, na hivyo akalelewa na bibi yake.

Akiwa katika malezi ya bibi, alipata ujauzito na hilo likamlazimu kutafuta maisha kwingineko.

Kipindi hicho alikimbilia kwa mjomba wake kujistiri.

Huko alitafutiwa kazi ya ndani ili kujikimu kimaisha hadi alipojifungua.

Lakini kufikia mwaka mwaka 2010, alimpoteza bibi yake na muda mfupi baadaye, akakutana na mwanaume ambaye angemuita mume wake….nyonda mkalia ini.

Tofauti kidogo pengine na wengine ambao wanachukua muda kufahamiana, Marion na mwandani wake walikuwa wamejuana kwa siku tatu pekee.

Na hivyo ndivyo walivyoamua kuanza kuishi pamoja kama mke na mume hasa baada ya kumuarifu kuwa anatafua mtu wa kuishi naye.

Marion alikuwa na matumaini na ndoa yake, kama wanawake wengi, matarajio ya amani, upendo na maisha bora. Lakini haikuchukua muda kugundua kuwa aliingia kwenye shimo la mateso. Mume wake aligeuka mtu mwingine: mlevi, mwenye hasira, asiyejali familia, na hatimaye, mwenye mawazo ya mauaji.

Tangu mwanzo, maisha yalikuwa na panda shuka. Ujauzito wake wa kwanza ulifungua mlango wa mateso ya kimwili, kiakili na kihisia. Mtoto aliyezaliwa alikumbwa na matatizo ya kiafya, lakini mume wake hakuonekana kujali hata kidogo.

"Alianza kubadilika, akawa mara harudi nyumbani, anakuja akiwa mlevi, naenda kumtafuta baa, sio tena ile ndoa niliyotarajia," anasema Marion.

Pia unaweza kusoma:
.
Maelezo ya picha, Meresa, jirani ya Maron aliyemsaidia pakubwa wakati anapitia changamoto

Wakati huo, alifanikiwa kukutana na Meresa Achieng aliyegeuka kuwa rafiki yake wa dhati, aliyempa moyo na matumaini kwamba iko siku mambo yatakuwa mazuri.

Alipoanza kupata maumivu ya kujifungua alipokuwa mjamzito wa mtoto wake huyo wa kwanza, ambaye kwa mumewe ni wa pili, alimuarifu mume wake ambaye hakuwa karibu akaamua kujipeleka hospitali.

Alijifungua salama na mume wake alichofanya ni kumpa pesa za kupanda bodaboda wakati wa kurejea nyumbani lakini yeye mwenyewe akatokomea.

"Hivi ndio mtu akiolewa mumewe anafaa kumfanyia");