'Nilipenda kuwa wa kwanza kuleta mwanga katika kijiji chetu'
Sio kawaida kumuona mama wa makamu kufanya kazi juu ya paa la nyumba tena akiwa amevaa Hijabu lakini kwa Fatma Haji Juma kwake ni fahari.
Yeye ni miongoni mwa wanawake wa kwanza kuwa fundi wa umeme wa jua kisiwani Zanzibar, wanaojulikana kama solar Mamas.
Alipata ujuzi kutoka nchini India baada ya kupewa mafunzo na taasisi ya Barefoot
Fatma anasema ndoto yake imetimia na sasa anatumia ujuzi huo kuwafundisha wanawake wengine:
Mwandishi wa BBC , Esther Namuhisa ametuandalia taarifa hii:
Picha :Eagan Salla na Bosha Nyange