Zainab Mtima: Aeleza faida na changamoto za kuwa dereva taxi mwanamke Zanzibar
‘Mteja alitaka kunishika nikakataa akaniambia ana elfu kama nauli’ - Zainab Mtima, Dereva taksi mwanamke Zanzibar.
Visiwani Zanzibar kuna maeneo mengi ya kitalii ambayo kama mgeni utatamani kuyatembelea.
Zainab Mtima ni mmoja wa madereva ambao watakufikisha salama lakini licha ya kufikia kiwango hiki cha kuwa dereva mwanamke na dereva maarufu visiwani Zanzibar, amepitia mengi magumu na ya kukatisha tamaa.
Hii hapa ni hadithi yake baada ya kukutana na Mwandishi wa BBC Frank Mavura Unguja, Zanzibar