Je, utumiaji wa pilipili kali unaweza kuleta madhara kwa afya?

L

Chanzo cha picha, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, Je, pilipili inaweza kuuwa?
  • Author, Jessica Brown
  • Nafasi, BBC

Tambi za Asia Mashariki zimepigwa marufuku katika baadhi ya nchi za Ulaya kwa kuwa na pilipili nyingi. Je, chakula hicho kinaweza kuwa na hatari kwa afya?

Tambi kutoka Korea Kusini ziligonga vichwa vya habari hivi karibuni, wakati mamlaka ya chakula ya Denmark, ilipoeleza hatari inayoweza kusababishwa na chakula hicho.

Habari nyingine iliyozua vichwa vya habari ni kisa cha kijana mmoja nchini Marekani, ambaye alikufa baada ya kushiriki katika shindano la kula chakula chenye pilipili kali.

Mamlaka ya Viwango vya Chakula nchini Uingereza hauruhusu wazalishaji wa chakula kuongeza pilipili halisi kwenye vyakula, kwani huchukuliwa kuwa si salama.

Ingawa hakuna kikomo juu ya kiasi cha kutumia, inapokuwa kwenye mkebe kutoka kiwandani.

Pia unaweza kusoma

Pilipili inaweza kuleta madhara gani?

Denmark sio nchi ya kwanza kuonya dhidi ya kula chakula kilicho na viwango vya juu vya pilipili. Taasisi ya Kutathmini Hatari nchini Ujerumani (BfR), pia imeonya dhidi ya matumizi ya kupindukia ya pilipili.

“Tafiti zinaonyesha ulaji mwingi wa pilipili unaweza kusababisha kiungulia, tumbo kuchoma, kichefuchefu, kuhara na maumivu kwenye tumbo na kifua,” inasema taasisi ya BfR.

“Inaweza pia kusababisha joto na baridi kwa wakati mmoja, mabadiliko ya shinikizo la damu au kizunguzungu. Lakini bado hakuna taarifa za kutosha kufafanua ni kiwango gani hasa cha matumizi ya pilipili kinaweza kusababisha hayo kutokea.”

"Kwa sababu athari ya pilipili inaweza kutokea kwa viwango tofauti vya matumizi, kutoka mtu mmoja na mwingine, hivyo hakuna kipimo cha uhakika cha kujua ni kiwango gani kina athari kwa afya kwa watu wasio na uzio," anasema msemaji wa BfR.

Ila kulingana na taarifa kutoka BfR, makadirio ya ulaji unaoweza kuleta athari ni miligramu 0.5 hadi 1 au zaidi, inaweza kusababisha athari, kama vile hisia ya joto, shinikizo kwenye tumbo au kiungulia.

Na makadirio mengine yanaweka kiwango hatari cha pilipili kwa binadamu ni miligramu 500-5,000 kwa kila kilo ya uzito wa mwili. Hii ni sawa na karibu miligramu 35,000 za pilipili kwa mtu mwenye uzani wa kilogramu 70.

"Ulaji wa kuanzia miligramu 170, kuna athari mbaya zinaweza kutokea. Kuna kesi ya mtu kulazwa hospitalini baada ya kumeza takribani miligramu 600 za pilipili," BfR inasema.

Mtu huyo mwenye umri wa miaka 27, alikuwa akishiriki shindano la kula pilipili huko Berlin, Ujerumani, alikula pilipili hoho nne na vyakula vingine vyenye pilipili.

Saa mbili na nusu baada ya kula chakula, alianza kuhisi maumivu makali ya tumbo na uvimbe kwenye tumbo, na jioni alikwenda katika Hospitali ya Helios Berlin-Buch.

Madaktari walimnywesha dawa za kutuliza maumivu. Baada ya saa 12 tangu ale pilipili, alitapika na hali yake ikaanza kukaa sawa.

Pilipili inaweza kuuwa?

K

Chanzo cha picha, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, Athari ndogo ndogo za pilipili, kama kuwasha hazipaswi kuleta wasiwasi

"Pilipili inaweza kusababisha muwasho, usumbufu na maumivu," anasema Christian Moro, profesa wa sayansi ya dawa katika Chuo Kikuu cha Bond huko Australia.

"Ikiingia kwenye jicho, inaweza kuuma sana, na kusababisha uoni hafifu. Ukipaaliwa, inaweza kusababisha kukohoa kwa muda mrefu, na hata kuchochea magonjwa kama vile pumu."

“Lakini athari ndogo ndogo za pilipili, kama kuwasha hazipaswi kuleta wasiwasi,” anasema Moro.

"Pilipili huamsha mishipa yetu na hii ndiyo sababu ya kuhisi kama mwili wako unaungua, lakini ni hisia tu, na haituletei madhara yoyote," anafafanua.

"Nimeulizwa mara nyingi: Je, kula pilipili kunauwa");