window.__reverb = {}; window.__reverb.__reverbLoadedPromise = new Promise((resolve, reject) => { window.__reverb.__resolveReverbLoaded = resolve; window.__reverb.__rejectReverbLoaded = reject; }); window.__reverb.__reverbTimeout = setTimeout(() => { window.__reverb.__rejectReverbLoaded(); }, 5000);

Putin anaitayarisha Urusi kwa vita vya muda mrefu - ISW

Katika muhtasari wake wa hivi punde Taasisi ya Marekani ya Utafiti wa Vita (ISW) inachambua hotuba ya hivi punde zaidi ya Rais Vladimir Putin katika mkutano wa Baraza la Haki za Kibinadamu siku ya Jumatano.

Moja kwa moja

  1. Mkutano Mkuu wa CCM wafikia tamati,

    Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Dkt. Samia Suluhu Hassan

    Chanzo cha picha, CCM

    Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Mapinduzi CCM umemalizika leo katika mji mkuu wa Tanzania Dodoma ambapo rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan amepitishwa katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda wa miaka mitano.

    Sambamba na hilo, pia kumechaguliwa makamu mwenyekiti wa Bara na Zanzibar pamoja na wajumbe 40 wa Halmashauri Kuu kati ya 374 waliowania nafasi hizo.

    Rais Samia amesema uchaguzi huu ni sehemu ya maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

    “Ni wajibu wa kila mwanachama aliyeteuliwa na chama kugombea nafasi aliyoomba, kutambua kwamba lengo la uchaguzi uliokwisha kufanyika na utakaofanyika sio kutafuta ushindi wa mtu mmoja mmoja bali ni mkakati wa kujiimarisha na kujipanga kwa ajili ya kutafuta ushindi wa chama chetu kwa ajili ya chaguzi zijazo,” amesema rais Samia.

    Wakati hayo yakijiri, upinzani nchini Tanzania wamekuwa wakilalamika kukosekana kwa fursa sawa za kunadi sera zao ikiwemo kufanya mikutano ya hadhara.

    Maelfu ya wajumbe waliohudhuria Mkutano huo walijawa na hisia mchanganyiko huku baadhi yao wakihofia kuibuka kidedea katika uchaguzi uliofanyika.

    Katika mkutano huo, pia kumeshuhudiwa utekelezaji wa mabadiliko ya katiba ikiwemo kutoa fursa kwa viongozi kuvaa kofia mbili katika uongozi wa juu.

    ”Baada ya hatua hii ya rais Samia kuchaguliwa kuongoza chama chake kwa miaka mitano, hivi sasa shauku kubwa iliopo miongoni mwa wananchi ni je, ataendelea na safu yake ile ile ya uongozi au ataamua kupangua pangua.”

    Kwa upande wa wananchi, iwapo kutafanyika mabadiliko ya uongozi, matumaini yao ni kupata viongozi watakaoleta mabadiliko.

    Mwajuma Selema ambae ni mwanachama wa CCM anasema iwapo rais atapangua safu ya uongozi wa Chama, basi angetamani kuona rais Samia akiweka viongozi wenye utashi wa kupambana na rushwa.

    Nae John Bin John ambae ni mkazi wa Dodoma anasema, hana matumaini yoyote ya mabadiliko katika uchaguzi uliofanyika ndani ya chama tawala.

    ”Sina mategemeo yoyote kwa uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi, kwa sababu kinacholeta maana ya chaguzi ndani ya chama na wanaopanga safu ndani ya chama, ni kutafuta maisha bora kwa mtanzania, lakini kwa hatua tuliyonayo sasa hivi, ni kwamba wanapofanya chaguzi wanataka manufaa ya wao na familia zao, lakini sio kwa ajili ya watanzania,” amesema John.

    Mkutano huu unafanyika wakati ambapo katika siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa majibizano makali kati ya wana CCM kufuatia kauli ya aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho Dk Bashiru Ali iliyodaiwa kuikosoa serikali.

    Joseph Butiku, kutoka Taasisi ya Mwalimu Nyerere anasema hakuna mpasuko wowote nda.

    Hii ni hatua muhimu ya kujiimarisha kisiasa kwa chama tawala, lakini kwa upande wa upinzani, nyota inaonekana kuzidi kufifia.

    Jawadu Mohammed ambae ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa na uchumi anakiri kwa upinzani kutopewa fursa sawa lakini anasema bado wana nafasi ya kuweka mikakati, ikiwemo kufanya mikutano ya ndani na kuja na sera mpya.

    ”Kumekuwa na tatizo kwa vyama vya upinzani hapa Tanzania, ya kwamba, pamoja na mambo mazuri ambayo upinzani huonyesha, lakini upinzani wa Tanzania wamejielekeza zaidi kutumia madhaifu madogo na makosa ya CCM katika kujinadi kwa watanzania,” amesema Jawadu.

    Mjadala unaoendelea hivi sasa ni iwapo ongezeko la idadi ya wajumbe kutoka 30 hadi 40 kutaongeza ufanisi ndani ya chama hicho au la, ni suala la muda.

  2. Cristiano Ronaldo: Ureno yakanusha kuwa nahodha huyo alitishia kuondoka kwenye kikosi cha Kombe la Dunia

    w

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Shirikisho la Soka la Ureno (FPF) limekanusha kuwa Cristiano Ronaldo alitishia kuondoka kwenye Kombe la Dunia.

    Jarida la Ureno la Record linadai fowadi huyo, 37, alitoa tishio hilo baada ya kuambiwa hataanza mchezo wao wa hatua ya 16 bora dhidi ya Uswizi.

    Katika mchezo uliopita dhidi ya Korea Kusini, nahodha huyo wa Ureno alijibu kwa hasira alipotolewa. FPF ilisema: "Hakuna wakati ambapo Cristiano Ronaldo alitishia kuondoka katika timu ya taifa wakati wa kukaa Qatar."

    Ronaldo aliondoka Manchester United kwa makubaliano ya pande zote mbili kabla ya kwenda na Ureno kwenye ufunguzi wa Kombe la Dunia baada ya mahojiano yenye utata ambapo mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d'Or aliikosoa klabu hiyo.

    Ronaldo alitolewa nje ya uwanja katika mechi zote mbili za ufunguzi za Ureno na kocha Fernando Santos alisema "hakupenda" maoni ya Ronaldo alipotolewa tena wakati wa kushindwa kwa 2-1 na Korea Kusini katika kundi. Goncalo Ramos alianza badala ya Ronaldo dhidi ya Uswizi na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alifunga hat-trick katika ushindi wa 6-1

    Ronaldo, ambaye ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi Ureno (195) na mfungaji bora wa muda wote (118), alitumika kama mchezaji wa akiba katika mchezo huo lakini, baadaye alitoka uwanjani wakati wachezaji wenzake wakiendelea kusherehekea.

    "Cristiano Ronaldo anajenga rekodi ya kipekee kila siku katika huduma ya timu ya taifa na nchi, ambayo lazima iheshimiwe," iliongeza FPF. "Kiwango cha kujitolea kwa mchezaji aliyechezewa zaidi na Ureno kilionyeshwa tena - ikiwa ni lazima - katika ushindi dhidi ya Uswizi, katika hatua ya 16 ya Kombe la Dunia la 2022."

    Ureno itamenyana na Morocco katika robo-fainali siku ya Jumamosi.

  3. Griner: Urusi yamwachilia nyota wa mpira wa vikapu wa Marekani kwa kubadilishana na muuza silaha Bout

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Brittney Griner alihukumiwa miaka tisa na mahakama nchini Urusi mwezi Agosti

    Marekani na Urusi zimebadilishana nyota wa mpira wa vikapu wa Marekani aliyefungwa Brittney Griner na mfanyabiashara maarufu wa silaha Viktor Bout, aliyezuiliwa katika jela ya Marekani kwa miaka 12.

    Mabadilishano hayo yalipitishwa na Rais Joe Biden katika siku za hivi karibuni, vyanzo viliiambia CBS.

    Griner alikamatwa katika uwanja wa ndege wa Moscow mwezi Februari kwa kumiliki mafuta ya bangi na mwezi uliopita alipelekwa kwenye mahakama ya adhabu.

    Kufikia majira ya kiangazi utawala wa Biden ulikuwa umependekeza kubadilishana wafungwa, ikifahamu kwamba Moscow ilikuwa ikitaka kuachiliwa kwa Bout kwa muda mrefu.

    Viktor Bout aliuza silaha kwa wababe wa vita na serikali, na kuwa mmoja wa watu wanaosakwa sana duniani.

    Alipewa jina la "mfanyabiashara wa kifo" kwa kukimbia na bunduki katika miaka ya baada ya kuanguka kwa Umoja wa Kisovyeti, ushujaa wake ulisababisha kubuniwa kwa filamu ya 2005 ya Hollywood ya Lord of War, ambayo ilikuwa na msingi wa maisha yake.

    Kazi yake ya usiri ilikomeshwa na Marekani mwaka 2008, alipokamatwa katika hoteli moja katika mji mkuu wa Thailand Bangkok, hatua ilioikasirisha serikali ya Urusi.

    Alirejeshwa nchini miaka miwili baadaye na amehudumu miaka 12 iliyopita akiteseka katika jela ya Marekani kwa kula njama za kusaidia magaidi na kuwaua Wamarekani.

  4. Harmonize aomba radhi kwa wimbo wa bangi,

    Harmonize ni mmoja wa wanamuziki maarufu Afrika Mashariki

    Mwanamuziki wa Tanzania, Harmonize ameomba radhi kutokana na maudhui ya wimbo wake mpya unaoitwa 'Weed Language', akisema kuwa unakiuka maadili na utamaduni wa nchi yake.

    Wimbo huo unaohusu bangi, ni ushirikiano na msanii wa dancehall kutoka Jamaica Konshens na ulitolewa wiki iliyopita. Kiitikio cha sauti katika wimbo wote ni: "Unaitaje bangi katika lugha yako">Kisha inaorodhesha masharti ya dawa katika nchi tofauti. Baadhi ya maneno katika Kiswahili yanaelezea hisia zinazotokana na kuvuta bangi. Katika taarifa yao, mameneja wa Harmonize walisema wimbo huo umetolewa kwenye mitandao ya kijamii na badala yake maneno yake yatabadilishwa na maneno ambayo hayakidhi maadili ya Kitanzania.

    Utumiaji wa bangi ni kosa la jinai nchini Tanzania na hukuu ya kifungo cha maisha jela. Haya yanajiri siku moja baada ya mwanamuziki huyo kupewa onyo na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania.

    Harmonize pia alikutana na maofisa wa Baraza la Sanaa, Basata kabla ya kuomba radhi. "Uongozi mkuu wa Muziki wa Konde Gang music Wordwide unaomba radhi kwa maudhui ya wimbo wangu wa Weed Language.

    Wimbo huo umekwenda kinyume na maadili ya taifa letu,” taarifa ya mameneja wake ilisema. Hapo awali Harmonize alisema kuwa wimbo huo ni moja ya nyimbo kwenye mradi wake mwezi huu. Hapo awali mwanamuziki huyo aliitwa kwa madai, ambayo anakanusha, ya utumiaji wa bangi.

  5. Wawili wafariki katika ajali ya ndege katika Hifadhi ya Kitaifa ya Tsavo Kenya

    Watu wawili wamefariki baada ya ndege ndogo kuanguka eneo la Huri katika Mbuga ya Kitaifa ya Tsavo.

    Shirika la Huduma ya Wanyamapori (KWS) lilithibitisha kuwa ndege hiyo ilianguka katika eneo la Kone kando ya Tiva katika Mbuga ya Kitaifa ya Tsavo Mashariki, Alhamisi asubuhi.

    Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation nchini Kenya , ndege hiyo yenye nambari ya usajili ya Cessna 185 5Y-DHS, ilikuwa ikimilikiwa na David Sheldrick Wildlife Trust (DSWT) na ilianguka mwendo wa saa 7.15 asubuhi ilipokuwa katika doria huko Huri - mpaka wa kaskazini mashariki mwa mbuga hiyo.

    Miongoni mwa waliofariki wanasadikiwa kuwa ni baba na mwanawe, ambao majina yao bado hayajawekwa wazi.

    Roan Hartley, rubani mwanachama wa DSWT na jamaa wa wawili hao alithibitisha kisa hicho, akibainisha kuwa wawili hao walikuwa binamu zake.

    Timu za KWS na DSWT ziko katika eneo la tukio kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.

  6. TikTok yashtakiwa kwa madai ya kutolinda usalama wa watumiaji Marekani

    Tik Tok

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Programu maarufu ya mitandao ya kijamii ya TikTok imeshtakiwa na jimbo la Indiana la Marekani.

    Mwanasheria mkuu wake Todd Rokita ameishutumu kampuni mama ya TikTok ByteDance kwa kukiuka sheria za serikali za usalama wa watumiaji.

    Serikali inadai kuwa programu hiyo inashindwa kuwalinda vijana na faragha.

    Hatahivyo,TikTok ilisema inazingatia ustawi wa vijana katika sera zake na kwamba ina uhakika inaweza kukidhi wasiwasi wa usalama wa kitaifa wa Marekani.

    Indiana ilifungua kesi mbili Jumatano. Ya kwanza inadai kuwa programu husababisha watumiaji wachanga kutazama maudhui yasiyofaa. Katika malalamiko mengine, Bw Rokita pia anadai TikTok haifichui uwezo wa serikali ya China kupata habari nyeti za watumiaji.

    "TikTok ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo," kulingana na hati za korti. "Mradi TikTok inaruhusiwa kudanganya na kupotosha watumiaji wa Indiana kuhusu hatari kwa data zao, watumiaji hao na faragha yao ni mawindo rahisi."

    Malalamiko yanasema kwamba kanuni za programu hukuza aina mbalimbali za maudhui yasiyofaa, "yanayoonesha pombe, tumbaku na dawa za kulevya; maudhui ya ngono, utupu na maudhui ya kuchochea ngono; na lugha chafu."

    Pia inadai kuwa huwahadaa watumiaji wachanga kwa ukadiriaji wa umri wa miaka 12 na zaidi kwenye Apple na Google app store. Indiana inatafuta amri dhidi ya desturi zake na adhabu dhidi ya kampuni kwa "mwenendo wake usio wa haki na wa udanganyifu."

    Bw Rokita alisema kesi hizo ni za kwanza kuanzishwa na serikali ya Marekani dhidi ya ByteDance. Msemaji wa TikTok alisema "usalama, faragha na usalama wa jamii yetu ndio kipaumbele chetu cha juu". Programu ina vipengele vya kuzuia umri na udhibiti wa wazazi, kampuni ilisema, na kampuni inawekeza katika udhibiti zaidi wa maudhui. Kwa kuongezea, TikTok iliyosemwa ilikuwa na imani kuwa inaweza kushughulikia "masuala yote yanayofaa ya usalama wa kitaifa wa Marekani".

    Tangazo la kesi hizo limekuja baada ya majimbo mengine ya Marekani kutunga sheria ya kupiga marufuku TikTok.

    Texas, South Dakota na South Carolina zimepiga marufuku matumizi ya TikTok kutumika kwenye vifaa vya serikali ya jimbo. Mwezi uliopita, mkuu wa FBI alisema kuwa TikTok inaleta wasiwasi wa usalama wa taifa.

    Mkurugenzi wake Chris Wray aliiambia Kamati ya Usalama wa Ndani ya Bunge la Marekani ilisema sheria ya China kimsingi inazitaka kampuni "kufanya chochote ambacho serikali inawataka wafanye katika suala la kupeana habari au kutumika kama chombo cha serikali ya China." Utawala wa Biden umekuwa katika mazungumzo na maafisa wa TikTok kwa miezi kadhaa wakijaribu kufikia makubaliano ya usalama wa kitaifa ili kulinda data ya mamia ya mamilioni ya watumiaji wake nchini Marekani.

    TikTok pia inakabiliwa na changamoto za kisheria mahali pengine. Nchini Uingereza, kampuni hiyo ya mitandao ya kijamii inaweza kukabiliwa na faini ya £27m ($29m) kwa kushindwa kulinda faragha ya watoto wanapokuwa wanatumia jukwaa hilo.

  7. Putin anaitayarisha Urusi kwa vita vya muda mrefu - ISW

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Rais Vlir Putin

    Katika muhtasari wake wa hivi punde Taasisi ya Marekani ya Utafiti wa Vita (ISW) inachambua hotuba ya hivi punde zaidi ya Rais Vladimir Putin katika mkutano wa Baraza la Haki za Kibinadamu siku ya Jumatano.

    Ndani yake, rais wa Urusi alisema kwamba "operesheni maalum ya kijeshi" (kama Kremlin inavyoita vita dhidi ya Ukraine) ni "mchakato mrefu" na inapaswa kusababisha kupatikana kwa maeneo mapya. "Putin alijifananaisha na Tsar Peter I wa Urusi, akisema kwamba Urusi sasa inadhibiti Bahari ya Azov, ambayo Peter alipigania," wataalam wamesema wataalamu wa Marekani.

    "Kutajwa kwa historia ya kifalme ya Urusi kunaweka wazi malengo ya sasa ya Putin nchini Ukraine kama ya kibeberu na bado ni ya kiwango cha juu," muhtasari huo ulisema. "Putin anatayarisha hadhira ya ndani ya Urusi kwa vita virefu, vya kuchosha nchini Ukraine, ambavyo vinahitajika ili kuyateka maeneo mapya ya Kiukreni."

    Aidha, wataalam wa Marekani wanatilia maanani matumizi ya kwanza ya ndege zisizo na rubani za Shahed zilizotengenezwa na Iran nchini Ukraine katika kipindi cha wiki tatu zilizopita. Jeshi la Ukraine lilisema kuwa jeshi la Urusi lilizitumia tena Jumatano usiku kwa mashambulio katika miji kadhaa, pamoja na mikoa ya Dnieper, Kyiv, Poltava, Zhytomyr na Zaporozhye.

    "Vikosi vya Urusi vina uwezekano wa kubadilisha ndege zisizo na rubani kwa matumizi katika msimu wa baridi na kuna uwezekano wa kuzitumia zaidi katika wiki zijazo kushambulia miundombinu muhimu ya Ukraine," wataalam wa ISW waliandika.

  8. Muungano wa Azimio Kenya wafuta mkutano Sambamba wa siku ya Jamhuri

    .

    Chanzo cha picha, Raila Odinag/Twitter

    Maelezo ya picha, Raila Odinga katika mkutano wa hadhara

    Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya umeghairi mpango wa kuandaa sherehe sambamba ya Sikukuu ya Jamhuri katika uwanja wa Jacaranda.

    Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa Opiyo Wandayi alisema hafla hiyo ilisitishwa kwa sababu ya mazungumzo yajayo ambayo yatawaweka mbali viongozi wakuu wa chama.

    “Tungependa kutangaza kuwa chama cha Azimio La Umoja One Kenya Coalition hakitaandaa sherehe sawia na Siku ya Jamhuri mnamo Desemba 12, 2022 jinsi ilivyopangwa awali,” alisema Bw Wandayi.

    Bw Wandayi aliongezea: "Kama Azimio, tunaahidi kwamba tutaendelea kusimama pamoja na kupigana hadi utawala wa Ruto itekeleze mambo muhimu kwa watu."

    Mbunge huyo alisema Alhamisi kwamba mazungumzo ya hadhara yataendelea kote nchini.

  9. Vifo vya malaria vyapungua huku kukiwa na wasiwasi kuhusu matibabu - WHO,

    Vifo vya malaria vyapungu huku kukiwa na wasiwasi kuhusu matibabu - WHO

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Shirika la Afya Ulimwenguni linasema kuwa kesi na vifo vya ugonjwa wa Malaria vilibaki chini mwaka jana, baada ya kuongezeka kwa wasiwasi katika mwaka wa kwanza wa janga la Covid.

    Lakini, katika ripoti yake ya dunia ya malaria iliyotolewa Alhamisi, WHO ilionya kuhusu changamoto mpya ikiwa ni pamoja na kustahimili viua wadudu na upinzani wa vimelea kwa dawa zinazotumika kutibu malaria.

    Asilimia tisini na tano ya visa vyote vya malaria viko barani Afrika, huku watoto walio chini ya miaka mitano wakiwa hatarini zaidi. Licha ya usumbufu unaoendelea wa huduma za afya unaosababishwa na Covid-19, vifo vya malaria vilipungua mwaka jana na 6,000, hadi 619,000.

    Kesi mpya ziliongezeka kidogo hadi milioni 247, kiwango cha chini zaidi kuliko mwaka uliopita. WHO inasema matokeo hayo mazuri kiasi yanatokana na nchi kuimarisha mwitikio wao katika kuzuia, kupima na kutibu malaria.

    Lakini ongezeko la upinzani dhidi ya viua wadudu vinavyotumiwa kwenye vyandarua ni jambo linalotia wasiwasi - pamoja na mbu kubadilisha tabia zao, kuuma mchana, nje, ambapo wanaweza kuepuka vyandarua.

    Kwa hivyo ingawa WHO inasifu nchi zinazofanya kazi kwa bidii kukabiliana na ugonjwa wa malaria, hakuna nafasi ya kuridhika - bila juhudi mpya za kimataifa, malaria inaweza kukimbia kabla ya kampeni ya kuidhibiti.

    Unaweza kusoma;

  10. 'Hatari ya Urusi kutumia silaha za nyuklia imepungua' - Kansela wa Ujerumani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, kansela wa Ujerumani Olaf Scholz

    Hatari ya silaha za nyuklia kutumika katika mzozo wa Ukraine imepungua "kwa wakati huu", anasema Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.

    "Urusi imeacha kutishia kutumia silaha za nyuklia ili kukabiliana na jumuiya ya kimataifa kuashiria mstari mwekundu," Bw Scholz alisema.

    Siku ya Jumatano, Vladimir Putin wa Urusi alipendekeza kuwa Moscow ingetumia tu silaha za nyuklia kulipiza kisasi.

    Lakini Marekani ilishutumu maoni hayo kama "mazungumzo yasio na msingi".

    Katika mahojiano siku ya Alhamisi, Bw Scholz alisema kuwa ziara yake ya hivi majuzi nchini China imechangia "kukomesha" tishio la kuongezeka kwa nyuklia.

    Alisema kuwa yeye na Rais wa China Xi Jinping walikuwa wanakubaliana kwamba "silaha za nyuklia zisitumike" na kwamba nchi za G20 zimesisitiza msimamo huu.

    Kauli ya Kansela wa Ujerumani imekuja siku moja baada ya Rais Putin kusema kwamba hatari ya vita vya nyuklia "inaongezeka - itakuwa ni makosa kuificha".

    Akizungumza katika mkutano uliopeperushwa hewani na runinga ya baraza lake la haki za binadamu, kiongozi huyo wa Urusi alisisitiza kuwa Urusi "chini ya hali yoyote" haitatumia silaha kwanza na haitatishia mtu yeyote na silaha zake za nyuklia.

    "Sisis sio wendawazimu, tunafahamu silaha za nyuklia ni nini," alisema, na kuongeza: "Hatuko karibu kutembea dunia nzima tukinowa silaha hii kama wembe."

  11. Kenya yaahidi ufadhili wa masomo kwa watakaohudhuria siku ya Jamhuri

    Serikali ya Kenya imeahidi kutoa idadi ambayo haijabainishwa ya ufadhili wa masomo bila malipo kwa Wakenya ambao watahudhuria sherehe za Jumatatu ya Siku ya Jamhuri - kuadhimisha siku ambayo nchi hiyo lilijipatia uhuru mwaka wa 1963 na pia siku ambayo ikawa Jamhuri mwaka mmoja baadaye.

    Afisa kutoka wizara ya mambo ya ndani, Raymond Omollo, alitoa tangazo hilo alipokagua uwanja wa michezo katika jiji kuu la Nairobi, utakaoandaa hafla hiyo.

    Ufadhili wa masomo kuhusu kozi za vyeti vya teknolojia utatolewa kwa "mtu mzima yeyote anayestahiki anayehudhuria sherehe hizo ana kwa ana".

    "Hii katika nia ya kuifanya Kenya kuwa kipaji cha juu zaidi duniani na kikanda katika teknolojia na uchumi wa kidijitali," wizara ya mambo ya ndani iliongeza kwenye tweet.

    Kozi hizo za bila malipo zinatolewa "katika masuala ya teknolojia na mada ya uchumi wa kidijitali" wakati wa sherehe za mwaka huu, ilisema.

    Kiongozi wa upinzani Raila Odinga ametangaza mipango ya kufanya sherehe sambamba siku hiyo hiyo katika ukumbi mmoja jijini - takriban kilomita 18 kutoka mahali ambapo hafla rasmi itafanyika.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  12. Zaidi ya raia 130 wauawa na waasi wa DR Congo - UN

    .

    Chanzo cha picha, AFP

    Umoja wa Mataifa unasema maelezo yametolewa kuhusu mauaji ya watu wengi mwishoni mwa Novemba mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mikononi mwa waasi wa M23.

    Inasema uchunguzi umethibitisha vifo vya takriban raia 131 katika vijiji viwili - Kishishe na Bambo - katika wilaya ya Rutsuhuru mkoani Kivu Kaskazini.

    Umoja wa Mataifa unasema wahasiriwa walinyongwa katika kile kinachoonekana kuwa kulipiza kisasi mashambulizi ya sasa ya serikali.

    Hata hivyo, waasi wa M23, ambao wameteka miji kadhaa karibu na mpaka wa Rwanda na Uganda mwaka huu, wamekanusha kuwa wanashambulia raia.

    Soma zaidi:

  13. Mwanariadha wa Kenya apokea medali ya Olimpiki miaka 10 baadaye

    .

    Chanzo cha picha, NOCK-Kenya Media

    Maelezo ya picha, Pamela Jelimo alisema kusubiri miaka mingi ilikuwa chungu

    Miaka kadhaa baada ya kumaliza wa nne katika fainali ya mita 800 kwenye Michezo ya Olimpiki ya 2012 jijini London, Mkenya Pamela Jelimo amepokea medali ya shaba.

    Jelimo, almaarufu Eldoret Express, alipewa nishani hiyo kufuatia Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) kumuondoa Mariya Savinova wa Urusi kwenye mashindano hayo kutokana na ukiukaji wa matumizi ya dawa za kusisimua misuli mwaka wa 2015.

    Savinova alishinda medali ya dhahabu ya mita 800 mwaka wa 2012. Akizungumza na BBC, Jelimo alilaani matumizi ya dawa za kusisimua misuli katika michezo, akisema ni "tishio kwa mwanariadha kuendeleza ujuzi wake kitaaluma", "Hii ni kama ndoto. Hapo awali sikuamini niliposikia habari hizi njema. Hakika ni ndoto ya kila mwanariadha kushinda medali katika Olimpiki na nina furaha kuwa na wazazi wangu kunisindikiza na kushiriki furaha hii.”

    Sherehe ya aina hii inajiri wakati ambapo Kenya imeangaziwa kutokana na visa vingi vya utumiaji dawa za kusisimua misuli na hivi majuzi nusra ikumbane na marufuku ya kimataifa.

    Soma zaidi:

  14. Chanjo ya Ebola yawasili Uganda kwa majaribio

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Uganda ilithibitisha kuzuka kwa ugonjwa wa Ebola mnamo mwezi Septemba

    Waziri wa afya wa Uganda Alhamisi atapokea shehena ya chanjo ya Ebola ambayo itatumika katika majaribio ya kimatibabu.

    Nchi hiyo imethibitisha kesi 142, na vifo 56, tangu ilipotangaza kuzuka kwa aina ya Ebola ya Sudan mnamo Septemba.

    Katika ujumbe wa Twitter, msemaji wa wizara ya afya Emmanuel Ainebyoona alisema shehena hiyo itapokelewa kutoka kwa wawakilishi wa Shirika la Afya Duniani kwenye ghala karibu na mji mkuu, Kampala.

    Waziri wa afya anatarajiwa kutangaza tarehe ya kuanza kwa majaribio, shirika la habari la AFP linaripoti.

    Uganda haijasajili visa vipya vya ugonjwa wa Ebola kwa zaidi ya wiki tatu, hali inayoashiria kwamba mlipuko huo unaweza kuwa umedhibitiwa.

    Soma zaidi:

  15. Nafasi ya Rais wa Peru Pedro Castillo kuchukuliwa na Dina Boluarte baada ya kuondolewa madarakani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Dina Boluarte alisema atatawala hadi 2026

    Peru ina rais mwanamke kwa mara ya kwanza, baada ya rais wa zamani Pedro Castillo kuondolewa madarakani - saa chache baada ya kujaribu kuvunja bunge.

    Dina Boluarte – ambaye hapo awali alikuwa makamu wa rais - aliapishwa baada ya siku ya kushangaza huko Lima Jumatano.

    Mapema siku hiyo, Bw Castillo alisema anaondoa Bunge kisha awe na "serikali ya kipekee ya dharura".

    Lakini wabunge walipuuza hili, na katika mkutano wa dharura wakamshtaki.

    Kisha akawekwa kizuizini na kushtakiwa kwa uasi.

    Ripoti katika vyombo vya habari vya ndani zinasema alikuwa akielekea katika ubalozi wa Mexico katika mji mkuu alipokamatwa.

    Bi Boluarte, wakili mwenye umri wa miaka 60, alisema atatawala hadi Julai 2026, wakati ambapo muda wa urais wa Bw Castillo utakuwa umekamilika.

    Akizungumza baada ya kula kiapo cha kuwa rais, alitoa wito wa kufikiwa kwa mapatano ya kisiasa ili kuondokana na mzozo ambao umeikumba nchi.

    "Ninachoomba ni nafasi, wakati wa kuokoa nchi,"

    alisema.

  16. Mfululizo wa filamu ya Harry na Meghan katika mtandao wa Netflix wazinduliwa huku kukiwa na utata

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mfululizo wa filamu ya Harry & Meghan katika mtandao wa Netflix unaanza Alhamisi na vipindi vitatu hata baada ya kuzua gumzo kali kwa umma na kusababisha utata.

    Filamu hiyo inaahidi kufichua ukweli wa simulizi ya ndani ya jinsi Duke na Duchess wa Sussex walijiuzulu kutoka kwa wadhifa wao wa kifalme.

    Kionjo cha filamu hiyo kinarejelea "vita dhidi ya Meghan", huku Mwanamfalme Harry akizungumzia "kuvuja na... kuzua mambo" kama sehemu ya "mchezo mchafu".

    Jumba la kifalme la Buckingham bado halijajibu madai ya Sussex.

    Kutakuwa na uchunguzi mkali wa mfululizo wa filamu hiyo.

    Pia "kufichua" maisha ya Ikulu kumeahidiwa, huku Mwanamfalme Harry akizungumza juu ya "maumivu na mateso ya wanawake wanaoolewa katika taasisi hii", katika kumbukumbu dhahiri ya mkewe, Meghan, na mama yake, Diana, Princess wa Wales.

    Kionjo cha filamu inapendekeza kwamba itafichua simulizi ya ya mapenzi ya kati ya Mwanamfalme Harry na Meghan yalivyokua.

    Lakini pia itaonyesha mabadiliko ya uhusiano na vyombo vya habari na umma.

    Hili litakuwa toleo lao la matukio - na wengine wa Familia ya Kifalme wanaweza kuwa wakitazama ili kuona jinsi madai yanavyoenda, ikiwa kuna ushahidi wowote na kama wanapaswa kujibu rasmi.

    Pia unaweza kusoma:

  17. Mzozo wa DRC: Waasi wa M23 washutumu jeshi kwa mauaji ya raia

    .

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Maelfu ya watu wameyakimbia makazi yao kutokana na ghasia zilizotokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

    Kundi la waasi la M23 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limelaani "mauaji ya halaiki na mauaji yaliyolengwa" dhidi ya jamii ya Watutsi yanayofanywa na vikosi vya serikali na washirika wake eneo la mashariki.

    Lilisema kuwa vikosi vya muungano vya serikali Jumanne "vimevamia ngome zetu huko Bwiza na maeneo yaliyo karibu, kinyume kabisa makubaliano ya usitishaji mapigano ".

    Kundi la M23 limesema vikosi vinavyoshirikiana na serikali vimewaua raia wasio na hatia, kuharibu nyumba, kuwapora na kuwachinja ng'ombe wao, na kubainisha kuwa mashambulizi yanayoendelea yamesababisha raia kutoroka makazi yao na kujeruhi wengi.

    "Haya yanalenga mauaji ya Watutsi, na wale ambao wamekataa itikadi ya mauaji ya kimbari ya muungano wa serikali ya DR Congo, wakati jumuiya ya kimataifa na ya kitaifa ilisalia kimya, kutoka zama za kabla ya mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi. nchini Rwanda," ilisema katika taarifa.

    Kundi hilo limesema "halitasimama na kutazama" wakati raia wakiuawa, na kuongeza kuwa "iko tayari kuingilia kati na kukomesha mauaji haya ya kutisha".

    Jeshi halijatoa kaili yoyote kuhusu madai hayo lakini wiki iliyopita liliwashutumu M23 kwa kuua makumi ya raia katika mji wa Kishishe mashariki mwa nchi, jambo ambalo walikikana.

    Kauli ya M23 inakuja baada ya kundi hilo kukubali kujiondoa katika eneo linalokalia kimabavu kufuatia shinikizo la kudumu kutoka kwa serikali na jumuiya ya kimataifa kufuatia maazimio yaliyokubaliwa na wakuu wa nchi wakati wa mkutano wa hivi majuzi katika mji mkuu wa Angola, Luanda.

    Zaidi ya vikundi 50 vyenye silaha vya Congo vilivyohudhuria mazungumzo ya amani yaliyokamilika wiki hii jijini Nairobi pia vilitangaza kuwa vimekubali kuweka chini silaha zao.

  18. Samuel Bateman: Kiongozi wa dhehebu la kidini alikuwa na wake 20, FBI inasema

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Washiriki wa manisa la Fundamentalist Church of Jesus Christ of Latter-Day Saints (picha kutoka maktaba)

    Mtu anayejiita nabii nchini Marekani alikuwa na wake zaidi ya 20, baadhi yao wakiwa chini ya miaka 18, Shirika la Ujasusi la Mare

    ani (FBI) imesema.

    Samuel Rappylee Bateman alidai kuwa ni mapenzi ya Mungu kwake kushiriki tendo la ndoa na wake zake, FBI ilisema.

    Bateman, 46, alishtakiwa mwezi Septemba kwa kuharibu rekodi na kuzuia haki katika uchunguzi wa iwapo watoto walikuwa wakisafirishwa katika majimbo mbalimbali kwa ajili ya kufanya ngono.

    Maelezo hayo yanatoka kwa hati ya kiapo ya FBI iliyowasilishwa Ijumaa.

    Bateman alikuwa mshiriki wa zamani wa tawi la Kanisa la Fundamentalist Church of Jesus Christ of Latter-Day Saints (Kanisa la FLDS) - dhehebu lililojitenga la kanisa la Mormon - hadi alipoondoka na kuanzisha kikundi chake mwenyewe kilichogawanyika.

    FBI ilisema kwamba Bateman alisaidiwa kifedha na wafuasi wa kiume ambao pia walitoa wake zao na watoto wao kuwa wake za Bateman.

    Aliwaadhibu wafuasi ambao hawakumchukulia kama nabii, FBI ilisema.

    Mnamo Agosti, Bateman alikamatwa alipogunduliwa akisafirisha trela na wasichana watatu wachanga wenye umri wa kati ya miaka 11 na 14. Aliweka dhamana lakini baadaye alikamatwa kwa madai ya kuharibu rekodi na kuzuia haki ikitendeke.

    Mapema mwaka huu, wasichana tisa waliondolewa kutoka kwa utunzaji wa Bateman na huduma za watoto za Arizona, na kuwekwa katika nyumba za kikundi.

    Mnamo Novemba, wanane kati yao walikimbia kutoka kwa nyumba za kikundi.

    Mamlaka ya jimbo la Washington iliwafuatilia wakati afisa mmoja aliripotiwa kuona gari likiendeshwa na mmoja wa wake za Bateman, kulingana na hati ya kiapo.

    Dereva huyo na wake wengine wawili wa Bateman wameshtakiwa kwa utekaji nyara katika kesi inayoendelea ya jinai, FBI ilisema.

    Dereva huyo amesema alikua mmoja wa wake za Bateman alipokuwa na umri wa chini ya miaka 18, FBI ilisema.

    Alijifungua miezi saba baada ya kutimiza miaka 18, kulingana na hati ya kiapo.

    Katika mahojiano na FBI, hakuna msichana yeyote kati ya tisa waliowekwa nyumbani aliyetaja unyanyasaji wa kijinsia na Bateman, lakini katika majarida, walirejelea mwingiliano wa karibu naye, hati ya kiapo ilisema.

    Kanisa la FLDS limetajwa kama kikundi cha chuki na Kituo cha Umaskini cha Sheria Kusini.

    Mnamo mwaka wa 2011, kiongozi wa FLDS alihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kuwadhalilisha kingono wafuasi wawili wa umri mdogo aliowachukua kama bi harusi.

    Pia unaweza kusoma:

  19. Indonesia 'marufuku ya ngono': Mabadiliko ya kanuni za uhalifu yanatishia uhuru mwingine

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Kanuni ya uhalifu iliyorekebishwa ya Indonesia imeidhinishwa wiki hii na bunge

    Kanuni ya makosa ya jinai iliyorekebishwa ambayo imeidhinishwa wiki hii na bunge la Indonesia inaangaziwa sana katika mfumo wa sheria wa nchi nyingine.

    Vichwa vya habari kote ulimwenguni vinawaonya watalii wanaozuru Indonesia kwamba wanakabiliwa na kifungo cha hadi mwaka mmoja jela iwapo watakutwa wakifanya ngono au kuishi pamoja na mtu ambaye hawajafunga naye ndoa.

    Ghafla nchi ambayo kawaida husifiwa kama yenye demokrasia ya Waislamu wengi imejikuta ikishutumiwa kwa kuingilia kati maadili.

    Kwa kweli ni jambo ngumu, na "marufuku ya ngono" sio mabadiliko yanayosumbua zaidi Waindonesia wengi, ambao wanaona maeneo mengine ya kanuni hiyo yakitishia haki za binadamu na uhuru wa kujieleza.

    Indonesia ilirithi mfumo wake wa kisheria kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Uholanzi, na serikali zilizofuata zimetaka kuurekebisha, na kuufanya kuwa muhimu zaidi kwa nchi katika nyakati za sasa.

    Rasimu iliwasilishwa bungeni miaka mitatu iliyopita, lakini ilizua maandamano makubwa na ilisitishwa kwa ushauri wa Rais Joko Widodo.

    Kamati iliyopewa jukumu la kuitayarisha tena mwaka huu imesema kanuni iliyorekebishwa imebadilishwa ili kuzingatia baadhi ya masuala ya umma.

    Inapaswa pia kusisitizwa kuwa sheria mpya hazitaanza kutekelezwa kwa miaka mitatu, na kwamba zinaweza kupingwa katika mahakama ya kikatiba.

    Lakini kanuni hiyo bado inawatia wasiwasi Waindonesia wengi.

    Kwanza, kuhusu maonyo hayo kwa watalii.

    Wageni wanafungwa na sheria kama vile hiyo ya Indonesia, lakini masharti kwamba huwezi kufunguliwa mashitaka kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa au kuishi pamoja isipokuwa malalamiko yatakapowasilishwa na mtoto, mzazi au mwenzi wa mshtakiwa hufanya iwe vigumu sana kwa watalii kuathiriwa.

    Hili ni muhimu zaidi kwa jumuiya ya LGBTQ ya Indonesia, ambao hawawezi kuoa, na wanahofia sheria hiyo itatumika dhidi yao.

    Wengine wametaja hatari ya kifungu hiki kutumiwa vibaya katika malipo ya kibinafsi dhidi ya wanafamilia waliotengana, au na watu wenye imani za kihafidhina au za kidini ambao hawawezi kukubali mapendeleo ya mtindo wa maisha wa watoto wao.

    Lakini ni vifungu vingine vya kanuni mpya ambavyo vinatishia sana wale wanaohusika na uhuru wa raia.

    Soma zaidi:

  20. Vita vya Ukraine: Putin anaiandaa Urusi kwa vita vya muda mrefu vya ubeberu

    G

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Katika mkutano na Baraza la haki za binadamu, Putin alizungumzia huu ya malengo ya kuyataa maeneo ya Peter I – na yake

    Katika taarifa yake ya hivi karibuni kuhusiana na vita vya Ukraine, taasisi ya Marekani ya stadi za vita (ISW) umechambua hotuba ya hivi karibuni iliyotolewa na Rais Vlir Putin katika mkutano na Baraza la haki za Binadamu siku ya Jumatano.

    Katika mkutano hyo, rais wa Urusi alisema kuwa alisema kwamba "operesheni maalum ya kijeshi" (kulingana na jinsi Kremlin inavyoviita vita dhidi ya Ukraine) iko katika "mchakato mrefu " n ani lazima matokeo yake yawe kunyakuliwa kwa maeneo zaidi. "Putin alijifananisha binafsi na Tsar Peter I wa Urusi, akisema kwamba Urusi sasa inadhibiti Bahari ya ​​ Azov, ambayo Peter the Great pia aliipigania," wataalamu hao wa Marekani wanasema..

    "Kutajwa kwa historia ya ubeberu wa Urusi wazikunayaweka malengo ya sasa ya Putin kwa Ukraine kama bebeeru aliye wazi na mtu mwenye mawazo ya Kimaxisti ," ilisema taarifa.

    "Putin anawaandaa Warusi kwa ajili ya vita vya muda mrefu visivyoisha, vinavyohitajika kwa ajili ya kuyateka maenei ya Ukraine."

    Aidha, Wataalamu wa masuala ya kivita wa Marekani, walielezea kuhusu matumizi ya kwanza ya Urusi ya droni zilizotengenezwa na Iran katika vita vya Ukraine wiki tatu zilizopita. Jeshi la Ukraine lilisema kuwa jeshi la Urusi kwa mara nyingine tena lilitumia droni hizo katika mashambulio dhidi ya miji kadhaa, ikiw ani pamoja naDnieper, jimbo a Kyiv , Poltava, na majimbo ya Zhytomyr na Zaporozhye.

    “Huenda vikosi vya Urusi vimezibadilisha dronihizo kwa ajili ya kuzitumia katika hali ya hewa ya baridi zaidi na huenda wasizitumie zaidi katika wiki zijazo kuishambulia miundo mbinu ya muhimu ya Waukraine,” wamesema wataalamu wa vita wa marekani.

    Awali, jeshi la Ukraine lilisema kwamba Urusi ililazimika kuachana na matumizi ya droni zilizotengenezwa na Iran kwasababu sio nzuri kutumiwa katika hali ya hewa ya baridi. Sasa, huenda jeshi la urusi limeweza kutatua tatizo hilo.

    Awali wataalamu hao wa Marekani walisema kuwa ‘’jeshi la Urusi linategemea kwa kiasi kikubwa mifumo iliyotengenezwa na Iran kutokana na kuharibika kwa silaha zake za makombora yanayoongozwa,"

    Urusi na Ukraine: Mengi zaidi:

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine