"Sikujua kuwa nina uja uzito hadi nilipojifungua"

.

Chanzo cha picha, Bryony Mills-Evans

Mwanamke huyo hakujua kwamba alikuwa na mimba hadi baada ya kujifungua.

Alisimulia jinsi alivyojifungua peke yake katika saluni aliyofanyia kazi na kukata kitovu cha mtoto wake kwa mkasi.

Bryony Mills-Evans alisema hata hakujua kama alitaka watoto, lakini alijifungua akiwa na miaka 23 bila dalili zozote za ujauzito.

Mimba zisizoeleweka, ambapo mwanamke hajui hali yake hadi mwishoni mwa ujauzito au, kama ilivyo kwa Briony, hadi wakati wa uchungu, zimeelezewa na profesa mmoja wa masuala ya uzazi kuwa "nadra lakini si ya kipekee."

Baada ya kujua kwamba kuna mambo machache sana yanayojulikana kuhusu mimba hizo, Briony aliamua kusimulia hadithi yake ili wengine waliowahi kupata mimba hiyo wajue kwamba hawako peke yao.

Skip Iliyosomwa zaidi and continue reading
Iliyosomwa zaidi