Kipi ni marufuku kwa wanawake na wanaume katika sheria mpya kali za Taliban?

Chanzo cha picha, Getty Images
- Author, Ali Hussaini
- Nafasi, BBC
Serikali ya Taliban imeweka sheria mpya iliyopitishwa wiki iliyopita nchini Afghanistan na wanadai inalenga ‘kukuza wema na kuondoa uovu,’ lakini Umoja wa Mataifa unasema sheria hiyo inatisha.
Vipengele katika sheria hiyo ni pamoja na kupiga marufuku wanawake kuzungumza kwa sauti kubwa hadharani na kuonyesha nyuso zao nje ya nyumba zao.
Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa alionya siku ya Jumapili kwamba sheria hizi zinatoa "taswira yenye kutisha ya siku zijazo kwa Afghanistan."
Sheria hizo mpya tayari zimeidhinishwa na kiongozi mkuu wa nchi hiyo, Haibatullah Akhundzada.
Wizara ya Maadili, iliyokuwa ikijulikana rasmi kwa jina la Wizara ya Kueneza Wema na Kuzuia Uovu, ilisisitiza kuwa hakuna mtu yeyote ambaye anasameheka na sheria hizo.