Misaada yamiminika kwa mwanamke aliyetamani kufa kutokana na ugumu wa maisha

- Author, Mansur Abubakar
- Nafasi, BBC
Shamsiyya Abubakar alikuwa ameanza kupoteza matumaini - mdororo mkubwa wa uchumi nchini Nigeria ulimfanya ahangaike kila siku kulisha familia yake ya watu tisa.
Bi Shamsiyya , mama wa mtoto mchanga, aliiambia BBC kwamba matatizo yake yamepeleka akili yake kuwa na mawazo mabaya.
"Wakati mwingine najiambia; 'badala ya kuishi hivi, si ingekuwa bora kufa");