Kwanini Zelensky hawezi kuiachia Urusi eneo hili?

Chanzo cha picha, Getty Images
- Author, Paul Kirby
- Nafasi, Mhariri BBC
Hapo awali Vladimir Putin alikanusha kuhusika kwa njia yoyote katika unyakuzi wa eneo la Crimea mnamo Februari 2014, wakati makomando waliovalia sare za kijani kibichi walipoliteka bunge la eneo hilo na kutawala rasi hiyo.
Hatua ya "wanajeshi hao" iliashiria mwanzo wa vita vya Urusi dhidi ya Ukraine, ambavyo viliishia katika uvamizi kamili wa 2022.
Mustakabali wa Crimea sasa uko katikati ya mpango wa amani wa Rais Donald Trump na umemfanya Volodymyr Zelensky wa Ukraine kukataa kutambua udhibiti wa Urusi katika rasi hiyo.
Masharti kamili ya mpango wake hayajachapishwa, lakini ripoti zinaonyesha kuwa itajumuisha Marekani kutambua Crimea kama sehemu ya kisheria ya Urusi - de jure kwa Kilatini.
Kwa mujibu wa Trump, rasi ya kusini ya Ukraine "ilipotea miaka iliyopita" na "sio sehemu ya majadiliano" katika mazungumzo ya hivi punde kutafuta ya amani.
Lakini kwa Zelensky kuachana na Crimea kama sehemu isiyoweza kugawanyika ya Ukraine itakuwa ni kutojali.
Kwa maneno ya mbunge wa upinzani Iryna Gerashchenko "uadilifu wa eneo na uhuru ni mstari mwekundu kwa Ukraine na raia wake".
Trump alitoa hoja kwamba "ikiwa [Volodymyr Zelensky] anataka Crimea, kwa nini hawakuipigania miaka 11 iliponyakuliwa na Urusi");