Tetesi za soka Ulaya Jumapili: Bruno Fernandes na wachezaji wengine 5 kuondoka Man United

Chanzo cha picha, Reuters
Nahodha Bruno Fernandes, mshambuliaji wa Ureno mwenye umri wa miaka 30, ni mmoja wa wachezaji sita wa kikosi cha kwanza wanaotarajiwa kuondoka Manchester United msimu huu wa joto. (Football Insider)
Bayern Munich wanamlenga Eberechi Eze kama mbadala wa Florian Wirtz, Liverpool na Newcastle wanavutiwa na Joao Pedro na Manchester United tayari kuuza idadi kuu ya wachezaji wa kikosi cha kwanza.
Bayern Munich wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Crystal Palace na England Eberechi Eze, 26, baada ya kumkosa mshambuliaji wa Ujerumani anayekwenda Liverpool Florian Wirtz, 22. (Mirror),
Liverpool wamempa Wirtz wa Bayer Leverkusen kandarasi yenye thamani ya zaidi ya pauni 320,000 kwa wiki huku wakitarajia kukamilisha dili la mchezaji huyo. (Sky Sports Switzerland – in French), nje

Chanzo cha picha, Getty Images
Mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich pia wanavutiwa na winga wa Brighton na Japan Kaoru Mitoma, 28, na mshambuliaji wa AC Milan na Ureno Rafael Leao, 25. (Mirror)