Jinsi watoto wawili walivyompata mama yao, miaka 13 baada ya kupotea

xx

Chanzo cha picha, NARESH PARAS

Siku moja wakati wa majira ya joto mnamo Juni 2010, watoto wawili wa Kihindi waliondoka nyumbani kwao, wakiwa na hasira kwa wazazi wao kwa kuwapiga.

Ndugu Rakhi, 11, na Bablu, 7, walikuwa wamepanga kwenda kwa bau wao, ambao waliishi kilomita moja tu kutoka hapo. Lakini baada ya makosa kidogo njiani, walipotea.

Iliwachukua zaidi ya miaka kumi na mitatu kumpata mama yao Neetu Kumari kwa msaada wa mwanaharakati wa haki za watoto.

“Nilimkumbuka mama yangu kila siku,” Bablu, ambaye alilelewa katika vituo vya watoto yatima, alisema. "Nimefurahi sana kupata familia yangu."

Video ya kuungana kwao mwishoni mwa Disemba inamuonyesha Neetu akilia huku akimkaribisha Bablu, huku akimkumbatia kwa nguvu na kumshukuru Mungu kwa "kumpa furaha ya kumshika mwanawe tena."

Kisha Bablu anamkumbatia Rakhi, ambaye alikuwa amerejea siku mbili zilizopita. Ingawa ndugu hao wawili walikuwa wamewasiliana kwa miaka kadhaa, walikutana tena baada ya zaidi ya miaka kumi.

Kutenganishwa

Bablu na Rakhi waliishi katika jiji la kaskazini la Agra na wazazi wao Neetu Kumari na Santosh, ambao walifanya kazi kama vibarua wa kila siku.

Mnamo Juni 16, 2010, Neetu, ambaye hakuweza kupata kazi siku hiyo, alitoa hasira yake kwa Rakhi na kumpiga na koleo za chuma alizokuwa akitumia kupika.

Rakhi na Bablu waliondoka nyumbani baada ya mama kwenda nje kwa shughuli fulani.

"Baba yangu pia alikuwa akinipiga wakati mwingine, kama sikusoma vizuri, hivyo Rakhi alipokuja na kusema 'twende kuishi na Dadi', nilikubali," anasema Bablu.

Baada ya kupotea, dereva wa teksi wa baiskeli aliwapeleka kituoni.

xx

Chanzo cha picha, NARESH PARAS

Huko, watoto walipanda treni ambapo waligunduliwa na mwanamke anayefanya kazi katika shirika la watoto.

Treni ilipofika Meerut, mji ulio karibu kilomita 250 kutoka nyumbani kwao, aliwakabidhi kwa polisi, ambao waliwapeleka kwenye kituo cha watoto yatima cha serikali.

“Tuliwaambia tunataka kurudi nyumbani, tulijaribu kuzungumza nao kuhusu wazazi wetu, lakini polisi au maofisa wa kituo cha watoto yatima hawakujaribu kuitafuta familia yetu,” anasema Bablu.

Mwaka mmoja baadaye, ndugu pia walitenganishwa: Rakhi alihamishwa hadi kituo cha wasichana kinachosimamiwa na shirika lisilo la serikali karibu na mji mkuu wa India, Delhi.

Miaka michache baadaye, Bablu alihamishiwa katika kituo kingine cha watoto yatima cha serikali huko Lucknow, mji mkuu wa jimbo la Uttar Pradesh.

Ndugu wanakutana tena

Kila mara maafisa muhimu, wafanyakazi wa misaada au waandishi wa habari walipotembelea kituo cha watoto yatima, Bablu alikuwa akiwaeleza kuhusu Rakhi kwa matumaini ya kukutana naye.

Lakini haikuwa hadi 2017 ndipo ilifanyika. Mmoja wa walezi katika makao hayo mapya aliamua kumsaidia alipomwambia kwamba dada yake alikuwa amepelekwa kwenye kituo cha watoto yatima cha wasichana mahali fulani karibu na Delhi.

"Aliita vituo vyote vya watoto yatima huko Noida na Greater Noida (vitongoji vya Delhi), akawauliza ikiwa walikuwa na mtu anayeitwa Rakhi na baada ya juhudi nyingi, akampata," anasema Bablu.

"Nataka niiambie serikali kuwa ni ukatili kweli kuwatenganisha kaka na dada, kaka na dada wapangiwe vituo vya pamoja, sio sawa kuwatenganisha," anaongeza.

Wawili hao walipokutana, mara nyingi walizungumza kwenye simu. Lakini mazungumzo yalipogeuka kuwa kutafuta familia yake, Rakhi alisisitizaa.

"Miaka kumi na tatu sio kitu bure na nilikuwa na matumaini kidogo ya kumpata mama yangu," aliniambia.

Bablu hakuwa na shaka kama hiyo. "Nilifurahi sana kumpata Rakhi na nilikuwa na uhakika kwamba ningeweza pia kumpata mama yetu," alisema.

Bablu anasema katika moja ya sehemu alizokaa, mara nyingi alikuwa akipigwa na walezi wake na watoto wakubwa. Alisema alijaribu kukimbia mara mbili, lakini aliogopa na kurudi.

Rakhi, kwa upande wake, anabainisha kuwa shirika lisilo la kiserikali alikokulia lilimtunza vizuri sana. Ninamuuliza ikiwa anafikiria maisha yake yangekuwa tofauti ikiwa angebaki nyumbani.

"Nadhani chochote kinachotokea huwa ni bora kila wakati na labda nilikuwa na maisha bora zaidi mbali na nyumbani," anasema.

"Sikuwa wa kwao, lakini walinitunza vizuri sana, hakuna mtu aliyewahi kunipiga na nilitendewa vizuri. Nilisoma shule nzuri, nilipata huduma nzuri za afya na huduma zingine zote ambazo kupata karibu na jiji kubwa,” anaongeza.

Mwanaharakati aliyeileta familia pamoja

Mnamo Desemba 20, Naresh Paras, mwanaharakati wa haki za watoto wa Agra, alipokea simu kutoka kwa Bablu, ambaye sasa anaishi na kufanya kazi huko Bengaluru.

"Umeunganisha familia nyingi, unaweza kunisaidia kupata yangu");