Afcon 2023: Wanasoka wa Afrika wanaocheza uwanjani licha ya kuhatarisha maisha yao

Mchezaji mmoja alikosekana wakati wa michezo miwili ya kwanza ya Zambia kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika 2023, lakini kutochaguliwa kwa Enock Mwepu hakukuwa na uhusiano wowote na uwezo wake.
Badala yake, ni kwa sababu kiungo huyo, ambaye alikuwa nahodha wa nchi yake katika mechi mbili za kwanza za kufuzu mwezi Juni 2022, alilazimika kustaafu soka baada ya kugundulika kuwa na ugonjwa wa moyo.
Wakati huo, mnamo mwezi Septemba akiwa na miaka 24, aliugua nchini Mali na akafanyiwa vipimo aliporejea katika iliyokuwa klabu yake, Brighton ya Ligi Kuu ya Uingereza, na kupokea matokeo hayo mabaya zaidi ambayo hakuwahi kufikiria.
Seagulls walisema Mwepu atakuwa katika "hatari kubwa sana ya kupatwa na mshtuko mbaya wa moyo" ambayo inaweza kusababisha hata kifo ikiwa ataendelea kucheza.
"Ni pigo kubwa kwa Enock, lakini anapaswa kuweka afya yake na familia yake mbele," mkuu wa masuala ya tiba wa Brighton alisema wakati huo.
"Hili ni chaguo sahihi, ingawa ni vigumu kuacha mchezo anaoupenda."
Hata hivyo si uamuzi ambao wanasoka wote wa Afrika katika nafasi ya Mwepu wangefanya.
Miezi miwili tu iliyopita, mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ghana Raphael Dwamena alifariki dunia baada ya kuanguka uwanjani nchini Albania, alipochagua kucheza baada ya kutoa kifaa cha kupandikizwa cha kufuatilia mapigo ya moyo kila mara yaani cardioverter-defibrillator (ICD), kilichowekwa mwaka 2020, ambacho kingeweza kuzuia mshtuko wake mbaya wa moyo.
Kiungo wa kati wa Manchester United Christian Eriksen aliwekewa kifaa kama hicho baada ya kuzimia alipokuwa akiichezea Denmark kwenye michuano ya Euro 2020.
Moja ya vilabu vya zamani vya Dwamena, FC Zurich, iligundua matatizo ya moyo wake kwa mara ya kwanza mwaka 2017 na kushauriwa na wataalam mbalimbali na madaktari wa magonjwa ya moyo kwamba angeweza kuendelea - jambo ambalo alifanya - huku timu hiyo ya Uswisi Super League ikihakikisha kila mara ina kifaa cha kufanya moyo upige tena wakati akiwa uwanjani iwapo kutatokea dharura.
Lakini hakukuwa na kipengele kama hicho katika klabu ya Egnatia FC ya Albania, ambao hawakupata mawasiliano na BBC lakini wakaiambia Athletic mwaka jana kwamba walikuwa na furaha kwa Dwamena kucheza "ili mradi majaribio yote yalifanywa na klabu".
Cha kusikitisha ni kwamba mshambuliaji huyo wa zamani wa Black Stars hakuwa Mwafrika pekee aliyefariki uwanjani mwaka jana.
Kombe la Mataifa ya Afrika 2023
- P - Imecheza
- W - Imeshinda
- L - Imeshindwa
- D - Imetoka Sare
- GD - Tofauti ya bao
- Pts - Alama
-
-
Kundi A
Nchi P W L D GD Pts Equatorial Guinea 3 2 0 1 6 7 Nigeria 3 2 0 1 2 7 Ivory Coast 3 1 2 0 -3 3 Guinea Bissau 3 0 3 0 -5 0 -
13/01/2024, 20:00Ivory Coast 2-0 Guinea Bissau-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
14/01/2024, 14:00Nigeria 1-1 Equatorial Guinea-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
18/01/2024, 14:00Equatorial Guinea 4-2 Guinea Bissau-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
18/01/2024, 17:00Ivory Coast 0-1 Nigeria-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
22/01/2024, 17:00Equatorial Guinea 4-0 Ivory Coast-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
22/01/2024, 17:00Guinea Bissau 0-1 Nigeria-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
-
Kundi B
Nchi P W L D GD Pts Cape Verde 3 2 0 1 4 7 Misri 3 0 0 3 0 3 Ghana 3 0 1 2 -1 2 Msumbiji 3 0 1 2 -3 2 -
14/01/2024, 17:00Misri 2-2 Msumbiji-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
14/01/2024, 20:00Ghana 1-2 Cape Verde-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
18/01/2024, 20:00Misri 2-2 Ghana-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
19/01/2024, 14:00Cape Verde 3-0 Msumbiji-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
22/01/2024, 20:00Cape Verde 2-2 Misri-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
22/01/2024, 20:00Msumbiji 2-2 Ghana-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
-
-
-
Kundi C
Nchi P W L D GD Pts Senegal 3 3 0 0 7 9 Cameroon 3 1 1 1 -1 4 Guinea 3 1 1 1 -1 4 Gambia 3 0 3 0 -5 0 -
15/01/2024, 14:00Senegal 3-0 Gambia-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
15/01/2024, 17:00Cameroon 1-1 Guinea-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
19/01/2024, 17:00Senegal 3-1 Cameroon-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
19/01/2024, 20:00Guinea 1-0 Gambia-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
23/01/2024, 17:00Gambia 2-3 Cameroon-(Uwanja wa Bouaké)
-
23/01/2024, 17:00Guinea 0-2 Senegal-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
-
Kundi D
Nchi P W L D GD Pts Angola 3 2 0 1 3 7 Burkina Faso 3 1 1 1 -1 4 Mauritania 3 1 2 0 -1 3 Algeria 3 0 1 2 -1 2 -
15/01/2024, 20:00Algeria 1-1 Angola-(Uwanja wa Bouaké)
-
16/01/2024, 14:00Burkina Faso 1-0 Mauritania-(Uwanja wa Bouaké)
-
20/01/2024, 14:00Algeria 2-2 Burkina Faso-(Uwanja wa Bouaké)
-
20/01/2024, 17:00Mauritania 2-3 Angola-(Uwanja wa Bouaké)
-
23/01/2024, 20:00Angola 2-0 Burkina Faso-(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
23/01/2024, 20:00Mauritania 1-0 Algeria-(Uwanja wa Bouaké)
-
-
-
-
Kundi E
Nchi P W L D GD Pts Mali 3 1 0 2 2 5 Afrika Kusini 3 1 1 1 2 4 Namibia 3 1 1 1 -3 4 Tunisia 3 0 1 2 -1 2 -
16/01/2024, 17:00Tunisia 0-1 Namibia-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
16/01/2024, 20:00Mali 2-0 Afrika Kusini-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
20/01/2024, 20:00Tunisia 1-1 Mali-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
21/01/2024, 20:00Afrika Kusini 4-0 Namibia-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
24/01/2024, 17:00Namibia 0-0 Mali-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
24/01/2024, 17:00Afrika Kusini 0-0 Tunisia-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
-
Kundi F
Nchi P W L D GD Pts Morocco 3 2 0 1 4 7 DR Congo 3 0 0 3 0 3 Zambia 3 0 1 2 -1 2 Tanzania 3 0 1 2 -3 2 -
17/01/2024, 17:00Morocco 3-0 Tanzania-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
17/01/2024, 20:00DR Congo 1-1 Zambia-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
21/01/2024, 14:00Morocco 1-1 DR Congo-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
21/01/2024, 17:00Zambia 1-1 Tanzania-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
24/01/2024, 20:00Tanzania 0-0 DR Congo-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
24/01/2024, 20:00Zambia 0-1 Morocco-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
-
-
Hatua ya 16 Bora
-
27/01/2024, 17:00Angola 3-0 Namibia-(Uwanja wa Bouaké)
-
27/01/2024, 20:00Nigeria 2-0 Cameroon-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
28/01/2024, 17:00Equatorial Guinea 0-1 Guinea-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
28/01/2024, 20:00Misri 1-1 DR Congo7-8(Penati)(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
29/01/2024, 17:00Cape Verde 1-0 Mauritania-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
29/01/2024, 20:00Senegal 1-1 Ivory Coast4-5(Penati)(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
30/01/2024, 17:00Mali 2-1 Burkina Faso-(Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly)
-
30/01/2024, 20:00Morocco 0-2 Afrika Kusini-(Uwanja wa Laurent Pokou)
-
-
Robo- Fainali
-
02/02/2024, 17:00Nigeria 1-0 Angola-(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
02/02/2024, 20:00DR Congo 3-1 Guinea-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
03/02/2024, 17:00Mali 1-2 Ivory Coast-(Uwanja wa Bouaké)
-
03/02/2024, 20:00Cape Verde 0-0 Afrika Kusini1-2(Penati)(Uwanja wa Charles Konan Banny de Yamoussoukro)
-
-
Nusu- Fainali
-
07/02/2024, 17:00Nigeria 1-1 Afrika Kusini4-2(Penati)(Uwanja wa Bouaké)
-
07/02/2024, 20:00Ivory Coast 1-0 DR Congo-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
-
Nafasi ya 3 na ya 4
-
10/02/2024, 20:00Afrika Kusini 0-0 DR Congo6-5(Penati)(Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny)
-
-
Fainali
-
11/02/2024, 20:00Nigeria 1-2 Ivory Coast-(Uwanja wa Olympique Alassane Ouattara)
-
Hatari inayowatokea

Moustapha Sylla alifariki dunia Machi mwaka jana alipokuwa akiichezea timu ya Racing Club d'Abidjan ya Ivory Coast, nchi ambayo kwa sasa ni mwenyeji wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika inayoendelea.
Kama Dwamena, Sylla pia angefahamu kwamba alikuwa akihatarisha maisha yake kwa kuingia uwanjani, kwani beki huyo alitolewa katika ligi ya Mali mnamo 2022 baada ya uchunguzi wa lazima wa kiafya kabla ya msimu mpya kufichua hali yake.
Kifo chake, akiwa na umri wa miaka 21 tu, kilimsukuma nahodha wa zamani wa Ivory Coast Didier Drogba kutoa ombi kwa niaba ya wachezaji wote wa ligi ya ndani ya nchi yake baada ya kutokea kwa kifo cha tatu kutokana na ugonjwa wa moyo tangu 2019.
"Rambirambi kwa soka la Ivory Coast... vifo 3 vya wachezaji katika ligi kuu ya Ivory Coast katika muda wa chini ya miaka 4…," Drogba alichapisha ujumbe huo kwenye mtandao wa X, wakati huo ukijulikana kama Twitter.
"Ni lini kutakuwa na uchunguzi wa lazima wa kiafya kwa wachezaji "wataalamu"?... Kipimo cha damu, ECG [Echocardiogram], vipimo vya msongo wa mawazo? Dawa kwa ajili ya wachezaji zitafika lini">
Uchaguzi wa kikosi cha AFCON 2023 na ushirikishe
Kwa kutumia mtandao wetu, chagua timu yako unayoipenda ya Kombe la Mataifa ya Afrika kutoka kwenye orodha yetu na uishirikishe marafiki zako.
Chagua mbinu
Chagua Mlinzi
Michuano hiyo itajumuisha makundi sita ya timu nne (A-F) huku timu mbili za juu zikifuzu moja kwa moja hatua ya 16 ya mwondoano.
Timu hizo 12 zitaunganishwa na timu nne zilizoshika nafasi ya tatu bora kutoka makundi sita, zikiwa na vigezo vinavyozingatia matokeo sambamba baina ya timu na pili tofauti ya mabao.
Utafiti na Damilola Ojetunde, uliyofanyiwa kazi na Olaniyi Adebimpe na Umeandaliwa na Boaz Ochieng

Suala moja kuu ni kwamba moyo wa Kiafrika unaaminika kukabiliwa zaidi na matatizo ya moyo, huku timu ya utafiti wa kimatibabu ikiungwa mkono na shirikisho la soka duniani Fifa, mwaka 2009, ikiamua kwamba "wanariadha weusi wa Kiafrika wanaonekana kuwa na hatari kubwa ya kupatwa na magonjwa ya moyo wakati wa matukio ya michezo".
Suala lingine la msingi ni kukataa kwa baadhi ya wachezaji wenye matatizo ya moyo kutii ushauri wa matibabu.
Daktari wa Afrika Kusini Lervasen Pillay ni mtu ambaye anajua hili vizuri sana, baada ya kuwashauri wanasoka watano tofauti kuacha kucheza kwa sababu ya matatizo yanayohusiana na moyo.
"Sio mazungumzo rahisi kamwe, kwa sababu mtu amekuwa akifanya kazi hii kwa miaka 10-15 na sasa umempa habari ya kusema, 'Sikiliza, huwezi kufanya hivi tena, unahitaji kuwa na mpango mwingine wa maisha', " Dkt Pillay aliiambia BBC Sport Africa.
"Wachezaji kandanda wengi hawajaanzisha Mpango Mwingine wanapokuwa na umri wa miaka 25, na mazungumzo mara nyingi yanatokana na swali hilo kamili: 'Nitafanya nini ikiwa nitaacha kucheza soka">Soma kuhusu mtazamo wetu wa viambatanishi vya nje.