Je,huyu ndiye mtu mrefu zaidi duniani?

TH

Niliposikia fununu za mshindani mpya wa mwanaume mrefu zaidi duniani kaskazini mwa Ghana, niliamua kujua kama ni kweli. Tatizo pekee? Kumpima.

Hospitali ya eneo la kaskazini mwa Ghana ilimwambia Sulemana Abdul Samed mwenye umri wa miaka 29 wakati wa uchunguzi wake wa hivi majuzi kwamba alikuwa amefikia urefu wa 9 ft 6in (2.89m).

Hii ingemfanya kuwa mtu mrefu zaidi duniani, lakini kulikuwa na  changamoto - kliniki ya vijijini haikuweza kuwa na uhakika wa urefu wake kwa sababu haikuwa na zana sahihi za kupimia.

Alipogunduliwa na ugonjwa wa gigantism(Unaomfanya kua kwa kiasi kikubwa) miaka michache iliyopita, kijana huyo alikuwa akihudhuria miadi ya kila mwezi ili kukabiliana na matatizo ya kuishi kama jitu alipoombwa kusimama moja kwa moja dhidi ya fimbo ya kupimia.

Muuguzi aliyeshtuka alimwambia: "Umekua mrefu kuliko mizani."

Aliyejulikana zaidi na kila mtu kwa jina lake la utani Awuche, linalomaanisha "Twende" kwa Kihausa, alifurahishwa na tamasha aliyokuwa akisababisha.

Hakushangaa kusikia yeye ni mrefu zaidi, ikizingatiwa kuwa hajawahi kuacha kukua - lakini ilisababisha mshangao kwa wafanyikazi, ambao hawakuwa wamejiandaa kwa hali kama hiyo.

Muuguzi wa zamu akamwita mwenzake, ambaye naye alimwita mwingine kuomba msaada. Muda si muda kundi la wauguzi na wasaidizi wa afya walikusanyika ili kutatua kitendawili cha kuamua urefu wake.

Mmoja alipendekeza watafute nguzo na kuitumia kama nyongeza juu ya fimbo yao ili kupima urefu wake - na hivi ndivyo walivyofikia makadirio yao.

 

  'Bado anakua'

Nilipokutana na Awuche miezi michache iliyopita nilipokuwa nikisafiri kaskazini mwa Ghana, ambapo umaarufu wake ulikuwa umeenea katika nyanda za eneo hilo, sikuwa na kanda ya kunipimia ili kuthibitisha urefu wake.

Kwa hivyo ili kusuluhisha suala hilo - na nikiwa na mkanda wa kupimia futi 16 - nilirudi katika kijiji cha Gambaga wiki iliyopita.

TH

Mpango ulikuwa ni kumfanya aegemee ukuta, aweke alama kwenye utosi wa kichwa chake kisha atambue urefu wake kwa kutumia mkanda wa kupimia.

"Jinsi wanavyonipima, siwezi kusema kila kitu ni sawa," Awuche alikiri - akifurahishwa na mpango wangu wa kupata kipimo kamili.

Alionekana kuwa mrefu kuliko nyumba nyingi za jirani yake, lakini baada ya utafutaji mzuri tukapata jengo linalofaa na ukuta wa kutosha. 

Alivua viatu vyake – pati pati  kubwa zilizotengenezwa maalum kutoka kwa matairi ya gari na akapigilia misumari pamoja na mfanyakazi wa eneo hilo kwa kuwa ameshindwa kupata viatu vya kumtosha

Mmoja wa majirani zake alipanda juu ya stuli ya  mbao ili kufikia urefu wa Awuche ili aweze kuweka alama kwenye ukuta kwa kipande cha makaa.

Baada ya kuthibitisha mstari, tulinyoosha utepe wa kupimia kwa uthabiti kutoka kwa mstari uliowekwa alama hadi chini huku Awuche akitazama kwa hamu.

TH

"Awuche, tepi ya kupimia inasoma 7ft 4in," nilisema.

Akiwa na  tabasamu lake lisilo na kifani, alijibu: "Wow, kwa hivyo inamaanisha nini");