WARIDI WA BBC: Nilishauriwa ‘kuzaa’ mapema ili kupona ugonjwa wa Endometriosis

Chanzo cha picha, Ritha Mwambene
- Author, Martha Saranga
- Nafasi, BBC Swahili
Ritha Mwambene, Mtanzania ambaye akiwa na umri wa miaka 18 alianza kupata dalili za maumivu yasiyo ya kawaida tangu alipopata hedhi kwa mara ya kwanza.
“Nimekuwa katika jamii ambayo unaambiwa kwamba ni kawaida mwanamke kupata maumivu anapokuwa katika hedhi’’
Kwa mara ya kwanza alipovunja ungo aliona ni hali ya kawaida hadi pale alipotimiza umri wa miaka 18 ndipo alianza kuona kwamba hilo halikuwa jambo la kawaida.
Alikuwa akiingia hedhi hadi siku 7 na huku akiwa mgonjwa sana na kupata damu nyingi.
Hali hii ilimsababishia kuwa mgonjwa haswa hali iliyomlazimu yeye pamoja na mama yake kuanza kwenda hospitali tofauti kutafuta majibu ya tatizo lake.