'Nilienda nyumbani kwa likizo ya Krismasi, lakini badala yake, 'nikakeketwa'

A photo of Catherine Meng’anyi

Chanzo cha picha, Catherine Meng’anyi

Maelezo ya picha, Catherine Meng'anyi
  • Author, Sandrine Lungumbu
  • Nafasi, BBC World Service

Catherine Meng'anyi wakati huo akiwa na umri wa miaka kumi na miwili alienda nyumbani kwa likizo ya Krismasi na familia yake, kama ilivyokuwa kila mwaka, lakini safari hii ilibadilisha maisha yake milele.

Bila yeye kujua, wazazi wake walikuwa wamepanga kwamba afanyiwe "ukeketaji" na mhudumu wa afya katika eneo analotokea nchini Kenya.

Onyo: Simulizi hii inazungumzia kwa undani ukeketaji.

Kukua katika mji mkuu, Nairobi, Catherine alidhani alikuwa salama kutokana na baadhi ya mila na desturi za jadi zilizofanywa mijini na vijijini.

Anasema hakuwa anafikiria kwamba angekuwa miongoni mwa wasichana ambao wamepitia ukeketaji; Wazazi wake walikuwa wameelimika vizuri, waliishi na walifanya kazi mjini.

Skip Iliyosomwa zaidi and continue reading
Iliyosomwa zaidi