'Alijiona kama Mfalme': Tafrija zilizosababisha anguko la Diddy

P. Diddy

Chanzo cha picha, Getty Images

Kuna wakati mwaliko wa tafrija iliyoandaliwa na Sean “Diddy” Combs ilikuwa moja ya tiketi zilizotafutwa sana katika tasnia ya burudani.

Kukiwa na orodha za wageni zilizojumuisha Justin Bieber, Mariah Carey, Paris Hilton na Jennifer Lopez, ilikuwa ni nafasi ya kuchangamana na baadhi ya watu mashuhuri wakubwa.

Jay-Z na Beyonce hata walitoa muziki mpya kwenye hafla zake.

"Wakati Diddy anapokukonyeza na kusema njoo kwenye kitengo cha watu mashuhuri, ulijua utakuwa na usiku mwema sana," Rob Shuter, ambaye alifanya kazi kama mtangazaji wa rapa huyo katika kilele cha umaarufu wake, aliiambia BBC News katika mahojiano maalum.

Sasa mteja wa zamani wa Bw Shuter ameketi katika seli ya jela ya Brooklyn, umbali mfupi kwa gari kutoka Hamptons, ambapo hapo awali alikuwa akisimamia tafrija za watu mashuhuri.

Kuanguka kwa Bw Combs kutoka kwenye neema imekuwa haraka, na kesi kubwa ya jinai ya shirikisho ikimshtaki kwa biashara ya ngono na njama ya ulaghai.

Zaidi ya kesi kumi na mbili za kiraia pia zimewasilishwa, zikimtuhumu nguli huyo wa muziki kwa unyanyasaji, ubakaji na unyang'anyi wa kingono. Wakili mmoja alisema anawakilisha zaidi ya waathiriwa 100 wanaodai walidhulumiwa kingono.

Rapa huyo mzaliwa wa Harlem amekanusha mara kwa mara makosa yoyote, iwe kuhusiana na madai ya jinai. Wawakilishi wa mwanamuziki huyo walikataa kutoa maoni kuhusu hili.

Lakini hapo awali, Erica Wolff, wakili anayemwakilisha Bw Combs, aliviambia vyombo vya habari Didy "kwa msisitizo na kimsingi" anakanusha madai hayo. Alisema ni "uongo na kashfa".

Anatarajiwa kuanza kusikilizwa kwa kesi yake Mei 2025.

Unaweza kusoma
Sean "Diddy" Combs alikua "mfalme wa karamu wa New York"

Chanzo cha picha, Getty Images

Bw.Shuter, ambaye alimfanyia kazi Diddy kuanzia 2002-04, alisema Bw.Combs alikuwa katika wakati muhimu sana katika kazi yake alipoanza kufanya kazi kwa mwanamuziki huyo.

Bw.Combs alikuwa ameanzisha Bad Boy Records mwaka wa 1993, lebo ambayo iliwakilisha baadhi ya majina makubwa katika hip hop, ikiwa ni pamoja na wasanii kama Notorious B.I.G. na Usher.

Mnamo 1998, aliunda safu ya mavazi ya Sean John ambayo baadaye ikawa jambo la kitamaduni.

Kuanzia hapo, aliingia kwenye manukato, pombe na hata kuanzisha kampuni ya vyombo vya habari, na kuwa mwenyeji wa maonesho mengi ambapo alivumbua talanta mpya na kuwafanya watu kuwa nyota.

Bwana Shuter alisema kuwa alipojiunga na ulimwengu wa rapper huyo kwa mara ya kwanza, Bwana Combs alitaka kubadilisha utu wake na kuinua kazi yake, akitafuta kutumia karamu zake kujiweka katikati ya tasnia ya burudani.

Bw. Shuter alisema Bw.Combs alihangaishwa sana na mamlaka na alitaka sana kubaki maarufu, akieleza kuwa nyota huyo alipenda kupigwa picha na alitaka kuonesha mtindo wake wa maisha.

Ilikuwa kazi ya Bw Shuter kusaidia kumuweka "Diddy" juu.

Alisema hajawahi kushuhudia upotovu wowote wa kingono. "Nimeona kukosekana kwa usawa wa madaraka," alisema. "Kile ambacho sijaona ni kile kinachodaiwa sasa, ambacho ni cha kutisha."

"Sababu ya yeye kuwa maarufu anachofikiria ni Diddy. Kuanzia dakika anapoamka hadi dakika ya kwenda kulala,” Bw Shuter aliiambia BBC News. "Mapenzi ya Diddy ni Diddy."

Pia anadai Bw Combs pia alivutiwa sana na familia ya kifalme ya Uingereza. Bwana Shuter alisema anakumbuka aliombwa zaidi ya mara 10 kuwapigia simu Prince Harry na Prince William na mialiko ya karamu, akijitolea kugharamia safari zao, malazi na hata kulipia usalama wao.

Katika nyumba yake ya kifahari ya New York, rapper huyo aliweka picha za wakuu, Bwana Shuter alisema, akielezea: "Alijiona kama mfalme kwa hivyo inaeleweka kabisa kwamba alipenda kuwa na wakuu wawili katika wasaidizi wake."

Harry na William hawakukubali mwaliko kutoka kwa Bwana Combs, aliongeza.

Bw.Shuter (anayeonekana kushoto) aliambatana na Mr Combs kwenye hafla mbalimbali, ikiwemo hafla ya hadhara ambapo rapper huyo aliwataka wengine kwenda kupiga kura katika uchaguzi wa 2004.

Chanzo cha picha, Getty Images

Lakini kusema "hapana" kwa nguli huyu wa muziki haikuwa jambo ambalo wengine wengi walifanya.

"Kila mara kulikuwa na bunduki karibu na Diddy," Bw Shuter alisema, akielezea mashine za ukaguzi katika nyumba yake ambavyo vinafanana na vile vya uwanja wa ndege. "Ilikuwa ajabu."

Bwana Shuter alielezea silaha za moto kwenye nyumba ya rapper huyo. Katika makazi yake ya binafsi, walinzi walikuwa na bunduki kwenye vifundo vyao.

"Huwezi kuwa Diddy ... isipokuwa watu walio karibu nawe wawe wamefungwa. Hakukuwa na mtu karibu naye aliyekuwa mzembe.”

Tafrija za mavazi meupe zilikuwa na mabaya, mashtaka yanadai

Katika eneo la Los Angeles, rapper huyo aliishi kwenye kile kinachojulikana kama eneo ghali zaidi ya Beverly Hills.

Uzio wa juu huruhusu watu mashuhuri kujificha kutoka kwenye macho ya nje.

Milango mirefu ya mali ya Bw Combs ina mwenge inayowaka mchana na usiku.

Majirani waliiambia BBC mara kwa mara waliita polisi kuhusu tafrija zake.

Ombi la uhuru wa habari la BBC limefichua kuwa maafisa walitumwa kwaenye karamu katika jumba la P Diddy mara 14 katika kipindi cha miaka saba.

Katika mtaa ambao busara na faragha ni muhimu sana, hakuna aliyetaka kutajwa jina, lakini majirani walieleza faraghani kwa BBC walichoshuhudia, wakisema kuwa wamechoshwa na kusumbuliwa na walichokiona.

"Kwa miaka sita au saba ilikuwa sherehe tu, karamu, karamu," jirani mmoja alisema, akiongeza kuwa aliona wanawake saa zote "wakitoka na kuketi mitaani, hawakujua walikuwa wapi".

Alisema walionekana "wamepotea" na "nguo zao za ndani zilionekana".

Watu mashuhuri kama Paris Hilton na Kim Kardashian walikuwa miongoni mwa waliohudhuria hafla ya White Party ya 2006.

Chanzo cha picha, Getty Images

Jumba la kifahari la Bw Combs huko Beverely Hills lilikuwa moja ya kumbi kadhaa alizotumia kuandaa "White Party" yake ya kila mwaka, hafla kuu ambayo alishikilia kutoka 1998 hadi 2009.

Alianza karamu katika eneo la kipekee la Hamptons la New York kwa kanuni kali ya mavazi meupe yote, akiwaleta pamoja matajiri wa pesa wa zamani wa East Hampton na nyota wanaochipukia wa hip hop.

Bwana Combs aliwahi kuelezea sherehe kama njia ya kuvunja vizuizi vya rangi na vizazi.

Lakini sherehe kali zaidi ya mwaka ilikuwa "kiashiria" ambacho kiliruhusu tabia "mbaya", kesi ya hivi karibuni inadai.

Katika kesi iliyowasilishwa wiki hii, mwanaume ambaye alikuwa na umri wa miaka 16 wakati huo, alielezea furaha ya kupata kuhudhuria "White Party" ya kwanza ya Bw Combs mwaka 1998.

Akiwa anaingia kwenye jumba la kifahari la Hamptons, aliona watu mashuhuri na wasimamizi wa burudani huku na kule. Katika kesi hiyo, alisema anaamini kuwa sherehe hizo zinaweza kufungua milango kwa tasnia ya muziki.

Alisema alikuwa akielekea bafuni ndipo alipokutana na rapper huyo. Walianza kuongea kisha wakahamia sehemu nyingine ya faragha. Hapo ndipo Bw Combs aliposema kuwa kijana huyo alikuwa na "mwonekano" sahihi na anaweza kumgeuza mtu yeyote kuwa nyota, mashtaka yanasema.

Kisha mambo yakageuka. Bw Combs ghafla aliamuru mvulana huyo wa wakati huo ashushe suruali yake ili Bw Combs amchunguze na kumgusa, ilielezwa.

Kulingana na kesi hiyo, Bw Combs alisema ilikuwa "ibada ya kupita" na "njia ya kuwa nyota". Pia inadai kwamba alisema ilikuwa njia yake ya kujithibitisha, akimuuliza kijana: "Je, hutaki kuingia katika biashara");